Habari za Punde

Mkutano wa wazi wa kutoa elimu ya katiba na umuhimu wa wananchi kushiriki, katika utungaji wa sheria Chanjamjawiri, Pemba

 SHEHA wa shehia ya Matale wilaya ya Chakechake Mkubwa Hamad Hassan, akifungua mkutano wa wazi wa kutoa elimu ya katiba na umuhimu wa wananchi kushiriki, katika utungaji wa sheria, ulioandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, na kufanyika skuli ya Chanjamjawiri shehiani humo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 MRATIBU wa mkutano wa wazi wa kuwaelewesha wananchi, umuhimu wa kushiriki kwenye utungaji wa sheria na katiba, kwa wananchi wa shehia ya Matale wilaya ya Chakechake Pemba, Khalfan Amour Mohamed na kufanyika skuli ya Chanjamjawiri wilayani humo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 WATENDAJI wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, wakifuatilia igizo lililoandaliwa na Kampuni ya Jufe Film Production ya Wete, kikiongozwa na Mwinyi Mpeku, lililoelezwa umuhimu wa kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria watoto wanaobakwa au kulawitiwa, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 BAADHI ya vijana na watoto wa shehia ya Matale wilaya ya Chakechake, waliohudhuria mkutano wa wazi wa kuelezwa umuhimu wa kushiriki kwenye utungaji wa sheria na katiba, ulioandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, na kufanyika skuli ya Chanjamjawiri wilayani humo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 WASANII wa kampuni Jufe Film Production ya Wete, wakiongozwa na Mwinyi Mpeku (mwenye kofia nyekundu) wakifanya igizo, lenye kuonyesha umuhimu wa wananchi kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria, mara watoto wanapolawitiwa au kubakwa, igizo hilo linafanyika skuli ya Chanjamjawiri na liliandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, (Picha na Haji Nassor, Peemba). 
WASANII wa Kampuni wa Jufe Film Production ya Wete, wakiwa pamoja na waandishi wa habari na watendaji wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, wakiwa kwenye picha ya pamoja, mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa wazi wa kuwaeleza wananchi umuhimu wa kushiriki katika utungaji wa katiba na sheria, uliofanyika skuli ya Chanjamjawiri, (Picha na hisani ya Jufe Film Production).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.