Habari za Punde

Ligi Kuu ya Zanzibar kanda ya Pemba: Shaba yauzima Mwenge yailaza 3 -0


NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.

KINYANGANYIRO cha kuwania nafasi nne za juu katika ligi kuu ya Zanzibar kanda ya Pemba, bado imezidi kuwa ngumu kwa vilabu ambazo vipo katika nafasi hiyo, kufuatia wavuvi wa kojani Timu ya Shaba kufanikiwa kuuzima mwenge kwa bado 3-1.

Mchezo uliopigwa katika uwanja wa michezo Gombani Huku ukishuhudiwa na mashabiki wengi wa soka, kutokana na timu hizo kujenga uhasama kila zinapokutana.

Shaba imeshuka uwanjani ikiwa na kisasi na mwenge kwa madai imeifanyia fitina hadi kutolewa katika mashindano ya kombe la Mapinduzi mwaka huu.

Mchezo huo uliochezeshwa na mwamuzi Hassan Abdalla Geri, huku ukionekana kutaka kumshinda katika dakika za mwisho, kufuatia wachezaji wa timu hizo kuanza kutembezeana buti na kushindwa kuwaonya kwa kadi za manjano.

Kipindi cha kwanza kilianz akwa kasi kubwa huku kila timu imkihitaji ushindi, ambapo shaba imeshuka kiwanjani ikiw ana alama 29 ikishika nafasi ya tano, Mwenge ikiwa na alama 35 ikishika nafasi ya pili.

Shaba waliweza kupata bao la kwanza kupitia kwa Omar Shamte dakika ya 21, bao lililodumu kwa dakika nne tu kufuatia mchezaji Yussuf Said kuisawazishia Mwenge dakika 24.

Kuingia kwa goli hilo pia liliweza kudumua kwa dakika nne tu, kufuatia mchezaji Salim Juma Ali, alipoweza kuwanyanyua mashabiki wa shaba na kuanza kurindima uwanjani hapo, baada ya kuipatia shaba bao la pili dakika 28.

Kuingia kwa magoli hayo mwenge na shaba ziliweza kucheza kwa umakini mkubwa, kwa kila timu kutokuruhusu goli jengine mlangoni mwake, huku kuyafanya magoli hayo kudumu hadi kipindi cha kwanza kinamalizika.

Kipindi cha pili kilirudi kwa kasi kubwa, huku mwenge wakiutawala sana mchezo katika kipindi hicho, kwa kutaka kusawazisha goli, lakini ngome za walinzi wa timu hizo kuwa imara.

Hata hivyo mabadiliko ya wachezaji wa timu hizo, yaliweza kuisaidia shaba dakika ya 81 walipopata penant ambapo mchezaji Salim Juma Ali alipobeba jukumu hilo, kwa kufanikiwa kuipatia shaba goli la tatu na mchezaji huyo kutimiza magoli 9 aliyofunga hadi sasa.

Kwa matokeo hayo shaba imefikisha alama 32, mwenge ikibakiwa na alama 35, ligi hiyo itaendelea tena leo (kesho) kwa timu ya Opec kuwakabili chipkizi katika uwanja wa Gombani.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.