Na Abdullah Mfaume, wilaya
ya kasakazini b
Mkuu
wa wilaya ya Kaskazini B bw.Rajab Ali Rajab amewataka wananchi wanaohama katika
nyumba za kiwanda cha sukari Mahonda kuwacha kuzifanyia hujuma nyumba hizo ili
ziwe katika hali ya usalama.
Wito
huo ameutowa huko Mahonda Kizota wakati alipokuwa akizungumza na wananchi
wanaondelea kuka a katika nyumba hizo.
Amesema
ana taarifa za kina za kuwa nyumba zilizohamwa zinafanyiwa hujuma kama vile
kutolewa nyaya za umeme,madirisha na kung’olewa milango kwa hivyo kila
aliyefanya hivyo atakapobainika hatuwa za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Rajab
amesema si jambo la busara na ni kinyume na nidhamu za makaazi kufanya vitendo
hivyo hata kama wanaofanya hivyo walifanya matengenezo lakini ni wazi gharama
za matengenezo waliyofanya hayalingani na thamani ya muda walioishi katika
nyumba hizo.
Nae
katibu tawala wa wilaya ya Kaskazini B Makame Machano haji amewataka wananchi
wanaoendelea kukaa katika nyumba hizo za starling wajiandae na kuhama kwani nyumba zote zinatakiwa
zirejeshwe serikalini.
Amesema
anafahamu kuwa ni jambo gumu wananchi
kuhama katika nyumba hizo kwa kuwa tayari wameshazowea kukaa lakini hakuna budi
kufuata agizo kama serikali inavyoelekeza.
Amewafahamisha
wananchi hao kuwa kuamriwa kuhama katika
nyumba hizo si jambo la uonevu au kuchikiwa na serekali bali sheria na
utaratibu ndivyo vinavyoelekeza.
Ameongeza
kuwa serekali ya wilaya ya kaskazini b itaendelea kuwahuduma wananchi hao kama
kawaida bila ya kuwabaguwa kwani seriskali haina chuki na mtu na itaendelea
kuwapenda wananchi wake.
Sheha
wa shehia ya Mahonda, Alhaj Bakari Juma amesema pamoja na vitendo vya uhalifu
vinavyo fanywa pia kumekuwa kukifanywa uharibifu wa mazingira kama vile kukatwa
miti na uchimbaji wa mchanga katika maeneo ya nyumba hizo.
Nao
wananchi waliohama na wanaoendelea kukaa wamekiri kuwepo kwa uharibifu huo na
kuitaka serikali isimamie utaratibu ikiwemo
muda wa kuhama waliobakia na kuwapa taarifa mapema itakapofika wakati wa
kuondoka na kuzingatia matumizi ya
taasisi za maendeleo na za kidini kama vile msikiti,skuli,madrasa na visima.
Jumla
ya kaya 41 zilizotakiwa kuhama katika awamu
ya kwanza tayari zimeshatekeleza agizo hilo na kwa sasa kaya 118
zimebakia na kuendelea kuishi bila ya kujuwa khatma yao itakuwa lini lakini
wameshapewa tahadhari siku yoyote wakitakiwa kuhama na wao watekeleze agizo hilo.
No comments:
Post a Comment