Habari za Punde

DKT. MPANGO AWASILISHA TAARIFA YA HALI YA UCHUMI MWAKA 2017 NA MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA 2018/19

Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) akiwasilisha Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa katika mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa  wa mwaka 2018/19 Bungeni Jijini Dodoma ambapo kwa mwaka 2017 uchumi wa Tanzania ulikua kwa asilimia 7.1.
Baadhi ya viongozi na Maafisa Waandamizi wa Wizara ya Fedha na Mipango wakifuatilia kwa makini Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa katika mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa  wa mwaka 2018/19 iliyokuwa ikiwasilishwa na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (hayupo pichani), Jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (kushoto) na Naibu wake Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), wakifurahia jambo Bungeni Dodoma baada ya  kuwasilishwa kwa Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa katika mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa  wa mwaka 2018/19 ambapo vipaumbele  vya sasa ni pamoja na mazingira wezeshi ya ufanyaji wa biashara, viwanda vya kukuza uchumi na kufungamanisha ukuaji wa uchumi na Maendeleo ya watu.
Kamishna wa Bajeti wa Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Mary Maganga (kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) Bw. Pius Maneno (wa pili kulia) na Mkaguzi Mkuu wa Ndani Bw. Mohamed Mtonga, wakiwa katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma baada ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, kuwasilisha Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa katika mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa  wa mwaka 2018/19.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Susana Mkapa, (kushoto) na Kamishna Msaidizi wa Sera wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. William  Mhoja wakipeana mikono  katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma baada ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango(Mb), kuwasilisha Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa katika mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa  wa mwaka 2018/19 ambapo Tanzania kwa mwaka 2017 mfumuko wa bei ulikua kwa wastani wa asilimia 5.1.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Prof. Florens Luoga, akizungumza jambo na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Bi. Sarah Cooke  baada ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango kuwasilisha Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa katika mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2018/19. ambapo moja ya vipaumbele vya sasa ni Kuimarisha utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo.

Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Wizara ya Fedha na Mipango  wakibadilishana mawazo katika viwanja vya Bunge  Jijini Dodoma baada ya  Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango,  kuwasilisha Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa katika mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa  wa mwaka 2018/19 ambapo Serikali imetenga takribani Sh. trilioni 12 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya Maendeleo.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha na Mipango)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.