Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein Azungumza na Uongozi wa Wizara ya Biashara Viwanda Zanzibar Ikulu.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Biashara na Viwanda  chini ya Waziri wake Balozi Amina Salum Ali ambaye alieleza kuwa kwa mwaka wa fedha 2017/2018, Shirika la Biashara la Taifa (ZSTC) lilikabiliwa na msimu mkubwa wa vuno la karafuu ambao haukuwahi kutokea kwa takriban mika 21 iliyopita.

Alieleza kuwa hata hivyo, Shirika lilifanikiwa kutekeleza jukumu lake la msingi la kununua karafuu kutoka kwa wakulima bila ya kusita.

Aliongeza kuwa Shirika la (ZSTC) lilijiwekea lengo la kununua jumla ya tani 6,770 kwa mwaka zenye thamani ya TZS 94.7 bilioni ambapo hadi kufikia Juni 2018, Shirika limenunua jumla ya tani 8,568 zenye thamani ya TZS 119.50 bilioni.

Aidha, alisema kuwa  katika kipindi cha mwaka 2017/2018, Shirika hilo limefanikiwa kuimarisha uzalishaji wa mafuta katika kiwanda cha Makonyo hali iliyopelekea kuongezeka kwa uzalishaji wa mafuta ya mimea kutoka Kgs 14,1713.6 kwa mwaka 2015/2016 hadi Kgs 59,524.05 kwa mwaka 2017/2018.

Pia, alielezea program kuu nne za Wizara hiyo kwa mwaka 2018/2019 ikiwemo uendeshaji na uratibu wa Wizara hiyo, maendeleo ya viwanda na ujasiriamali, program ya ukuzaji na uendelezaji biashara na program ya viwango na uthibiti ubora.

Nae Dk. Shein kwa upande wake aliupongeza uongozi wa Wizara hiyo pamoja na watendaji wake kwa kutekeleza vyema majukumu yao pamoja na kuendelea kusimamia vyema masuala ya biashara na viwanda kwa lengo la kuimarisha uchumi na maendeleo ya Zanzibar na wananchi wake.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.