Habari za Punde

Simba kukutana na Mabingwa Watetezi Timu ya Gor Mahia Katika Mchezo wa Fainali ya Kombe la SportPesa


Mashabiki wa Timu ya Simba wakiishangilia Timu yao wakati wa mchezo wao wa Nusu Fainali ya Michuano ya Kombe la Sport Pesa uliofanyika katika Uwanja wa Nakuru Kenya Timu ya Simba imeshinda kwa Penenti 
Mshabiki wa Timu ya Kakamega Homeboyz akiishangilia Timu yake wakati ikicheza na Mabingwa wa Tanzania Timu ya Simba katika Michuano ya Kombe la Sport Pesa uliofanyika katika Uwanja wa Nakuru Nchini Kenya. Timu ya Simba imeshinda kwa mikwaju ya Penenti. 
Mabingwa wa ligi ya Tanzania bara Simba wametinga fainali ya michuano ya Super Cup ya kampuni ya Sportspesa baada ya kuwacharaza Kakamega Homeboyz wa Kenya kwa mikwaju 5-4 ya penalti.
Watakutana na mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Kenya Gor Mahia ambao wameibuka washindi kwa kuwanyuka Singida FC wa Kenya 2-0.
Mabao hayo yamefungwa na Meddie Kagere. mechi za nusu fainali zilichezewa uwanja wa Afraha, Nakuru.
Simba walifika nusu fainali baada ya kuwaondoa Kariobangi Sharks wa Kenya. Singida FC walifika nusu fainali kwa kuwaondoa mahasimu wa jadi wa Gor Mahia AFC Leopards.
Kakamega Homeboyz ndio waliokuwa wamewatoa mashindanoni timu kongwe nchini Tanzania Yanga kwa kuipachika mabao 3-1 kwenye mechi ya ufunguzi.Jumla ya dola 57,500 zitashindaniwa katika mashindano hayo.
Mshindi wa mashindano hayo atasafiri hadi England kutoana jasho na Everton katika uwanja wao wa Goodison Park mwezi wa saba.
Bingwa mtetezi Gor Mahia ndiyo iliyocheza na Everton mwaka jana jijini Dar es Salaam ikapoteza kwa mabao 2-1, wafungaji wa Everton wakiwa ni mchezaji nyota wa zamani wa Manchester United Wayne Rooney na Kieran Dowell, naye Jacques Tuyisenge akaipa Gor Mahia bao lao moja.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.