Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Boniface akimkabidhi sare ya mmoja wa Wahitimu wa Mafunzo ya Wataalam wa kubeba Wagonjwa "Patient Transporter" Tunu Salum akipokea sare maalum inayowatambulisha Wataalam hao wa kubebea wagonjwa na kusafirisha
Mkurugenzi wa
huduma za Uuguzi MOI bwana Fidelis Minja akizungumza katika hafla ya kufunga
mafunzo ya kubeba na kusafirisha wagonjwa ambayo yamehituimishwa leo MOI.
Mkurugenzi Mtendaji
wa MOI Dkt Respicious Boniface (Aliyeketi katikati) na viongozi wengine
waandamizi wa MOI pamoja na kiongozi wa chama cha kuweka na kukopa cha wauguzi (TANA
Capt Adam Laeyna) wakiwa katika picha ya pamoja na wahitimu wa mafunzo ya
kusafirisha na kubeba wagonjwa.
Patrick
Mvungi- MOI
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa MOI Dkt Respicious Boniface amefunga
mafunzo ya wataalamu wa kubeba wagonjwa ‘Patient transporters’ .
Mafunzo
hayo yajulikanayo kama ‘Basic life support ‘ yamefanyika kwa miezi 6 na
wataalamu 12 wamehitimu ambapo lengo ni kuwapa mbinu za kuwasafirisha na
kuwabeba wagonjwa kwenda na kutoka maeneno mbalimbali kwa kuzingatia misingi ya
usalama wa mgonjwa.
Dkt.
Respicious Boniface amesema kwamba Taasisi ya MOI imewajengea uwezo wataalamu
hawa kwa lengo la kuhakikisha wagonjwa wanasafirishwa kwa kuzingatia misingi na
maadili ya afya na kuhakikisha wagonjwa wanakua kwenye mkono salama katika
kipindi chote wanaposafirishwa kutoka eneo moja kwenda eneo jingine.
“Mgonjwa
aliyefanyiwa upasuaji wa mgongo, nyonga ,magoti au anapata shida kupumua namna
yake ya kumsafirisha na kumbeba lazima iwe ya kisayansi na inahitaji
umakini mkubwa lasivyo mgonjwa anaweza kupata tatizo jingine au kufariki,
naamini mtatekeleza jukumu hili kwa umakini mkubwa kama
walivyojifunza” alisema Dkt Boniface
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa huduma za Uuguzi MOI Bwana Fidelis Minja amesema
wataalamu hawa wtajulikana kama patient transporters ambao pamoja na mbinu
nyingine wana utaalamu wa kumsaidia mgonjwa endapo atapata shida yoyote pindi
atakapo kuwa kwenye mchakato wa kusafiri kutoka eneo moja kwenda jingine.
“Hali
ya mgonjwa inaweza kubadilika muda wowote akiwa kwenye mchakato wa kuhamishwa
au kupelekwa eneo lolote la hospitali, kwamfano mgonjwa anatolewa wodini kwenda
kwenye kipimo kama MRI na njiani akapata ‘cardiac arrest’ wataalamu hawa
wanaweza kupatia huduma ya msingi kabla hajafika kwenye chumba cha dharura na
hivyo kuokoa Maisha yake” alisema bwana Minja.
Aidha,
Mkurugenzi wa tiba MOI Dkt Samuel Swai amesema uwepo wa wataalamu hawa
utasaidia wagonjwa kuwa salama kabla ya kufika kwenye eneo husika au kwa
daktari. Aliongeza kwamba hospitali nyingi zina changamoto ya ubebaji wa
wagonjwa kwa namna inayofaa na wakati mwingine wagonjwa wanapata matatizo
kwakubebwa katika namna isiyosalama.
Mwenyekiti
wa chama cha ushirika cha kuweka na kukopa cha wauguzi Tanzania (TANA SUCOSS)
Capt Adam Francis Leyna ameipongeza taasisi ya MOI kwa jitihada kubwa za
kuboresha huduma kwa wagonjwa na kuahidi kuendelea kufadhili mafunzo mengine
yenye tija kwa wauguzi wa MOI na kwa taifa.
Taasisi
ya MOI imekua ikiendesha mafunzo kwa wataalamu wake kwa lengo la kuhakikisha
watanzania wanapata huduma bora kwa kuzingatia msingi ya usalama wa mgonjwa.
No comments:
Post a Comment