STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 06.07.2018
RAIS wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, ameondoka nchini leo kuelekea Uingereza kwa
safari maalum ya wiki tatu.
Katika uwanja wa ndege wa
Kimataifa wa Abeid Amani Karume viongozi mbali mbali wa Serikali, vyama vya
siasa pamoja na wakuu wa vikosi vya
ulinzi na usalama wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar walimuaga Rais Dk. Shein.
Dk. Shein katika safari
hiyo, amefuatana na Mkewe Mama Mwanamwema Shein pamoja na Watendaji wengine wa
Serikali.
Wakati
huo huo,
Rais Dk. Shein amemtumia salamu za pongezi Rais wa Comoro, Azali Assoumani kwa
kutimiza miaka 43 tokea kupata Uhuru kwa Taifa hilo.
Salamu hizo zilieleza kuwa
kwa niaba yake Dk. Shein, wananchi pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
wanaungana pamoja na ndugu zao wa Comoro katika kusherehekea siku hiyo adhimu
ya uhuru wa Taifa hilo.
Aidha, katika salamu hizo,
Dk. Shein alimuhakikishia Rais Azali Assoumani kuwa Zanzibar itaendeleza
uhusiano na ushirikiano mkubwa uliopo kati yake na nchi hiyo pamoja na wananchi
wake sambamba na kuimarisha ustawi wa pande mbili hizo.
Dk. Shein alimtakia
kiongozi huyo na familia yake pamoja na wananchi wote wa Comoro kuendeleza
amani, upendo na utulivu walionao ili maendeleo yazidi kuimarika. Comoro ilipata
uhuru wake Julai 6 mwaka 1975 kutoka kwa koloni la Kifaransa.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment