Habari za Punde

TAMASHA la Utalii, Utamaduni, Biashara na Michezo lafikia tamati Fukwe za Vumawimbi Wilaya ya Michewen

 SHAKA Khatib Salim aliyeibuka mshindi wa kwanza katika mashindano ya Kuogelea umbali wa mita 800, akijinyakulia shilingi Milioni 1,000,000/= na kushinda wenzake 52 mashindano hayo yaliyofanyika katika Fukwe za Vumawimbi ikiwa ni kilele cha Tamasha la Utalii, Utamaduni, Biashara na Michezo Zanzibar .(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)


WACHEZAJI wa Ngoma ya Kubwaya kutoka Mkoani wakikomoana shetani, baada ya kupandisha wakati ilipokuwa ikipigwa ngoma hiyo, katika kilele cha ufungaji wa Tamasha la Utalii, Utamaduni, Biashara na Michezo, lililofanyika katika Fukwe za Vumawimbi .(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
NGALAWA inayojulikana kwa jina la Jali Muda inayoendeshwa na Nahodha Faki Khatoro, akiibuka mshindi wa kwanza katika mashindano ya Ngalawa, yaliyofanyika katika Fukwe za Vumawimbi ikiwa ni kilele cha Tamasha la Utalii, Utamaduni, Biashara na Michezo Zanzibar, mshindi huyo alijipatisha shilingi Milioni 1,000,000/=.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)


NA ABDI SULEIMAN, PEMBA

TAMASHA la Utalii, Utamaduni, Biashara na Michezo limemalizika rasmi Katika i Mkoa wa Kaskazini Pemba, kwa mbio za Baskeli, Mchezo wa Kuogolea na Resi za ngalawa kutawala katika ufungaji wa Tamasha hilo.

Mbio hizo za Baskeli zilizowashirikisha wasukuma Pedeli 40 kutoka Wilaya ya Micheweni na Wete, zilizoanzia katika Hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani hadi Konde zenye urefu wa kilomita 86.

Nafasi ya Kwanza katika mbio za baskeli ilikwenda kwa Othman Said Abdalla aliyejipatia shilingi Milioni 1,000,000/=, mshindi wa Pili alikuwa ni Yussuf Mwinyi Ginja aliyejipatia shilingi Laki 500,000/= nafasi ya Tatu ikaenda kwa Omar Khamis Abdalla aliyejipatia laki 300,000/= wote kutoka Tumbe ambao walitumia muda wa saa 2:21 wakitafautiana kwa sekunde.

Mchezo wa Kuogelea umewashirikisha Waogeleaji 52 wanaume 50 na wanawake wawili, aliweza kushindana kupiga mbizi umbali wa mita 800, ambapo Shaka Hatib Salim aliibuka na ushindi wa kwanza na kujinyakulia shilingi Milioni 1,000,000/=, nafasi ya pili ikaenda kwa Faki Omar Faki aliyejipatia Laki 500,000/= na fasi ya tatu ikaenda kwa Ali Hamad aliyejipatia Laki 300,000/= wote kutoka Maziwa ng’ombe.

Kwa upande wa resi za Ngalawa ambapo ngalawa 12 ziliweza kutega upepo katika Fukwe za Vumawimbi Wilaya ya Micheweni, huku Ngalawa yenye jina la Jali Mwendo inayoongozwa nahodha Faki Khatoro aliyejinyakulia shilingi Milioni 1,000,000/=, huku nafasi ya pili ikachukuliwa na ngalawa yenye jina la Babalo iliyoongozwa na nahoza Ali Shaame aliyejipatia shilingi laki 500,000/=, nafasi ya tatu ikachukuliwa na Ngalawa ya Mwendo Kasi inayoongozwa na Nahodha Said Abdi aliyejipatia shilingi Laki 300,000/=.

Mapema tamasha hilo liliingia dosora kufuatia washindi wa Baskeli kutokufurahia kitendo, kilichofanywa na Kampuni ya Rafiki Network wakati wa utoaji wa zawadi kwa washindi.

Kitendo hicho kiliwafanya washindi hao kutishia kurudisha fedha wazopewa na kampuni hiyo, kuwa ni kinyume na makubaliano ya awali ya zawadi za washindi.

Hali hiyo iliweza kumfanya Afisa Mdhanini Wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale Khatib Juma mjaja na Mkurugenzi kutoka Kamisheni Masoko wa kamisheni ya Utalii Zanzibar Dkt Miraji Ussi Ukuti kuingilia kati, juu ya mzozo huo ambao ulitishia hata mchezo wa kuongelea na mashindano ya ngalawa kutokufanyika, kutokana kitendo hicho cha Rafiki Network.

Baada ya kuingilia kati na kutuliza ghasia hizo na washiriki kukabidhiwa zawadi zao kama walivyokubaliana awali na Kampuni hiyo, pamoja na kutangazwa kwa zawadi za michezo ya kuogelea na mashindano ya Ngalawa, ndipo washiriki walipokubali kuingia baharini.

Akizungumza na wanamichezo katika ufungaji wa Tamasha hilo, Mkuu wa Wilaya ya Wete Abeid Juma Ali, alisema kufanyika kwa Tamasha hilo, kuendeleza kuvitangaza vivutio vya utalii vilivyopo kisiwani Pemba.

Alisema Kisiwa Cha Pemba kimejaaliw akuw ana vivutio vingi vya kiutalii, ambavyo bado havijatambuliwa na wageni wanaoingia Kisiwa Cha Pemba, hivyo alitaka kamisheni ya Utalii kuandaa matamasha mengine kwa lengo la kuvitangaza vizutio hivyo.

“Kufanyika kwa matamasha haya ni kutangaza utalii wetu wa kisiwa cha Pemba, utalii tunafahamu sote kama unachangia pato la taifa, amani na utulivu ndio kitu Pekee cha kufanya utalii utakambulika”alisema.

Hata hivyo aliwataka wananchi kuvitunza, kuvienzi na kuviendeleza vivutio vya utalii vilivyopo Pemba, sambamba na kuwataka wanamichezo Kulinda afya zao kwani michezo ni ajira kwa sasa.

Mkurugenzi wa Masoko Kamisheni ya Utalii Zanzibar Dkt Miraji Ussi Ukuti, alisema kamisheni ya Utalii itahakikisha inaliendeleza Tamasha hilo kila mwaka, ili kuvitangaza zaidi vivutio vya Utalii vilivyopo Kisiwani Pemba.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.