Na.Judith Mhina -Maelezo Dar.
Kitendo cha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kushtakiwa mara nyingi zaidi katika Mahakama ya Afrika ya Haki ya Binadamu ni
ushahidi tosha kuwa Serikali imetoa
uhuru wakushtakiwa kutokana na makubaliano
ya Kimataifa yaliyosainiwa na Serikali yenyewe.
Maneno hayo yamethibitishwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye amesema kuwa, Serikali itahakikisha Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu (AfCPHR) kuwa itatekeleza kwa ukamilifu
amri na hukumu mbalimbali zinazotolewa na mahakama kama ambavyo imeainishwa katika mkataba wa kuridhia mahakama hiyo.
Kutokana na taarifa iliyoripotiwa na gazeti la Mtanzania, toleo Na. 9013 la tarehe 25 Agosti 2018 lenye kichwa cha Habari “Tanzania
yaongoza kwa kushtakiwa Afrika ” ambapo Serikali ya Tanzania imedhihirika kuwa
na mashtaka 117 katika Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu yenye jumla ya
kesi 180.
Tanzania kama nchi ni kinara wa kulinda haki za binadamu Afrika Mashariki na kati na ndio maana Makamu wa Rais, Mhe Samia amesema “Serikali
itaendelea kushirikiana na mahakama hiyo katika kulinda haki hizo. Hivyo kitendo cha kuwa na mashauri mengi
zaidi katika mahakama hiyo inatokana na uelewa mkubwa wa wananchi katika
kutafuta haki zao pia urahisi wa kuifikia mahakama hiyo.
Uhuru wa kuishtaki Serikali upo katika nchi ambayo ina uhuru
wa kweli na Utawala wa Sheria na hili ni jambo muhimu sana Watanzania
kulifahamu. Nchi ambazo hazijali Haki za Binadamu huwezi kuishtaki Serikali,
ndio maana Tanzania imeridhia makubaliano mbalimbali ya Kimataifa na kikanda.
Baadhi ya mikataba hiyo ambayo imeandaliwa na Chama
Cha Wanasheria Tanzania Bara “ Zijue Haki za Binadamu, Sheria katika lugha rahisi ni kama vile “Tamko la Kimataifa la Haki za Binadamu la Mwaka
1948”. Tamko hili limekubaliwa na
kupitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 10 Desemba, mwaka 1948.
Hivyo, Tamko hilo ndilo chimbuko la kulindwa kwa haki za binadamu duniani kote. Tamko hili linajumuisha, kwa pamoja, aina zote za haki
za binadamu, yaani haki za kiraia na kisiasa, na haki za kiuchumi, kijamii na
kiutamaduni.
Tamko la Kimataifa la haki za binadamu ni “tamko” halina
masharti ya kuzibana nchi kutekeleza haki za binadamu kisheria. Pamoja na kuwa
halina nguvu kisheria. Tamko hili linaheshima kubwa sana kimataifa na nchi
nyingi wamelitambua na kuingiza kwenye katiba zao. Tanzania imefanya hivyo
katika Ibara ya 9 (f) ya Katiba ya nchi ya mwaka 1977.
Nyingine ni “Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa wa Mwaka 1966. Ambao ulipitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
mwaka 1966 na kuanza kutumika Machi, 1976. Tanzania imeukubali na kuuridhia
mkataba huo tarehe 11 Septemba 1976.
Kama nchi Tanzania ina jukumu la kuheshimu na kuwahakikishia
watu wote uwepo wa haki hizi bila ubaguzi wa aina yoyote, kama vile rangi,
kabila, lugha, dini, asili au utaifa wao; Kupitisha sheria na hatua nyingine za
kulinda haki zilizomo kwenye mkataba pale ambapo sheria au hatua zozote
hazijafanywa;
Aidha, sheria zimeweka
utaratibu kuhakikisha mtu yeyote aliyeingiliwa au kukiukwa kwa haki na uhuru
wake anapata ufumbuzi kama vile kulipwa fidia;
Kuhakikisha usawa kati
ya wanaume na wanawake katika kufaidi haki za
kiraia na kisiasa zilizoorodheshwa kwenye mkataba.
Vilevile, kuna Mkataba wa Kiafrika wa Haki za Binadamu na Haki za Watu wa Mwaka 1981 Mkataba huu ulipitishwa na wakuu wa nchi na serikali
za Umoja wa Nchi za Afrika (OAU), Nairobi – Kenya mwaka 1981.
Hadi leo nchi zote za Afrika ni wanachama wa Mkataba huu. Nchi wanachama zina wajibu wa kutambua haki, uhuru na wajibu uliomo kwenye
mkataba na kuchukua hatua za kisheria kuzipa nguvu haki. Mkataba wa Kiafrika wa
Haki za Binadamu na Haki za Watu unatambua na kulinda aina zote za haki za binadamu
yaani haki za kisiasa, kiraia, kiuchumi, kiutamaduni na kijamii.
Mfano wa haki za binadamu zinazotambuliwa na kulindwa kwa
Haki za Binadamu ni pamoja na Haki ya kutobaguliwa, usawa, haki ya Zijue Haki
za Binadamu 7 kuheshimiwa, haki na uhuru
ya kuabudu na kujumuika na wengine. Ulinzi wa Haki za Binadamu Mlinzi wa kwanza
wa haki hizi ni binadamu mwenyewe.
Akitembelea Mahakama hiyo Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt.Julius
Mashamba na Naibu wake Dkt Ally Possi, wametimiza wajibu wao wa kufuatilia mahakama
hiyo, kujua nini kimejiri ili kuhakikisha kila Mtanzania ana haki ya
kusikilizwa na kutendewa haki.
“Wengi wanaolalamika haki zao katika kesi za jinai hazijatekelezwa kwa namna kesi zilivyosikilizwa na kuchelewa kupata nakala za
mwenendo wa kesi ili wakati rufaa au kunyimwa msaada wa sheria” amesema Dkt. Mashamba ameongeza kuwa, jambo kubwa lililofanya kutembelea Mahakama hiyo ni wingi wa kesi hizo na hasa zikichukuliwa kama
zimekuwa zikifanana kwani wengi hudai kutopata masaa wa kisheria wakati mahakama
za ndani zilizotoa uamuzi wake.
Chimbuko na Utambuzi wa Haki za Binadamu kwa kipindi kirefu
haki za binadamu zimekuwepo na kuongoza maisha ya mwanadamu kulingana na asili
ya kila mwanadamu. Kukua na kutambulika kwa haki za binadamu kumepitia madaraja kadhaa kulingana na hatua kadhaa za kukua kwa jamii.
Kabla ya karne ya 19 haki hizi zilikandamizwa na kupuuzwa na
jamii, serikali iliyotawala katika jamii husika na wakati mwingine mataifa
yaliyoingia kutawala mataifa mengine.
Hali hii ililawalazimisha watetezi wa
haki za binadamu kufanya kazi ya ushawishi ili kuanza hatua ya kuainisha na kuzitambua haki za binadamu.
Hatua ya kwanza kabisa ya utambuzi wa haki za binadamu ilitokana na kuzidi kwa vitendo vya ubaguzi, ukatili, unyanyasaji, kutumikisha
watu kwa kuwaita watumwa na uonevu dhidi ya binadamu na matendo mengine ya aina
hiyo.
No comments:
Post a Comment