Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitembelea kiwanda cha kisasa cha kusindika kahawa cha AMIMZA cha mjini Bukoba Oktoba 9, 2018. Wapili kushoto ni Mkurugenzi wa kiwanda, Amiri Hamza na kushoto ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage. Wapili kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa .
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kuhusu usindikaji wa kahawa yenye viwango vya juu kutoka kwa Mkurugenzi wa Kiwanda cha kahawa cha AMIMZA kilichopo Bukoba, Bw. Amiri Hamza (wapili kushoto) wakati alipotembelea kiwanda hicho, Oktoba 9, 2018. Watatu kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage na wapili kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
No comments:
Post a Comment