JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
TUME YA TAIFA YA
UCHAGUZI
|
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
UTEUZI
DIWANI WANAWAKE VITI MAALUM
Kwa
mujibu wa Kifungu cha 86A (8) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Tume
ya Taifa ya Uchaguzi katika kikao chake cha tarehe 23 Januari, 2019 imemteua Ndg. FATUMA MICHAEL SHIJA kuwa Diwani wa Viti Maalum (CCM) katika
Halmashauri ya Manispaa ya Temeke.
Uteuzi
huu umefanyika baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Waziri mwenye dhamana ya
Serikali za Mitaa, ambaye kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 13(1) cha
Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, aliitaarifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi
uwepo wa nafasi hiyo wazi, kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) baada ya aliyeteuliwa
awali kufariki dunia.
Imetolewa
leo tarehe 23 Januari, 2019.
Dkt. Athumani J. Kihamia
MKURUGENZI
WA UCHAGUZI
No comments:
Post a Comment