Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein,akiweka jiwe la Msingi la Mradi wa Ujenzi wa Mnara wa Tangi la Maji Safi na Salama eneo la Mnara wa Mbao Kilimani Zanzibar, akiwa katika ziara yake Wilaya ya Mjini Unguja leo.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein amewaeleza wananchi wa
Mkoa wa Mjini kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itahakikisha inaukamilisha
mradi wa maji safi na salama ili changamoto ya uhaba wa huduma hiyo iwe
historia hapa Zanzibar.
Dk. Shein alisema kuwa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatafuta kila njia katika kuhakikisha
wananchi wa Zanzibar wanapata huduma ya maji safi na salama katika Mji Mkongwe
wa Zanzibar pamoja na maeneo ya Nambo ya Zamani.
Rais Dk. Shein
aliyasema hayo leo huko Saateni katika hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi Tangi
la Maji Saateni ambapo mapema aliweka jiwe la msingi Tangi la Maji Mnara wa
Mbao, Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi ikiwa ni mwanzo wa ziara yake ya
kutembelea Mikoa yote ya Zanzibar atakayoihimisha Februari 25 mwaka huu.
Katika maelezo yake,
Rais Dk. Shein alisema kuwa kila Awamu ya uongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar ilijitahidi katika kutatua tatizo la maji na kila kiongozi alifanya
wajibu wake juu ya kuwapatia wananchi huduma hiyo na hakuna aliyedharau.
Aliongeza kuwa katika
uongozi wa Awamu ya Saba juhudi hizo ziliendelea na kufanya kazi kubwa ikiwa ni
pamoja na kuanza kutafuta fedha, vifaa pamoja na wajenzi wa miradi na
miundombinu ya maji.
Alieleza kuwa mradi
huo wa maji ukikamila hali ya maji itakuwa ni bora kwani hizo zote ni juhudi za
Serikali katika kuhakikishwa wananchi wa Zanzibar wanapata maji safi na salama.
Alisema kuwa Serikali
inakwenda hatua kwa hatua na kuwasisitiza wananchi kuwa wastahamilivu kwani
mradi huo utamalizika na utakuwa mkombozi mkubwa kwa wananchi.
Rais Dk. Shein alisema
kuwa juhudi za makusudi kwa kushirikiana na washirika wa Maendeleo ikiwemo
Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB ambapo iliikopesha Zanzibar Dola milioni 21, Serikali ya Ras al khaimah imechimba visima
23, India imetoa kwa mkopo wa Dola milioni 92 pamoja na msaada kutoka Serikali
ya Japan wa Dola milioni 100 kwa ajili ya kuimarisha huduma hiyo ya maji.
“Hakuna dhiki wa dhiki
na badala yake baada ya dhiki faraji, hivyo wananchi endeleeni kustahamili
Serikali yenu haikupuuzini msinune hakuna mtu anetaka wananchi mpate tabu na
vizuri mjue kuwa hakuna mtu anaeweza kutatua tatizo hilo haraka haraka”,alisema
Dk. Shein.
Rais Dk. Shein
aliwataka wananchi kuachana na mambo mengi yanayosmwa na kunukuu maneno ya Rais
Salmin Amour Juma kuwa jambo la muhimu ni kuhakikiisha wanashika mpini yaani
wanashika Dola. “watasema mchana na usiku watalala ”,alisisitiza.
Aidha, Rais Dk. Shein
alieleza kuwa yote yanaofanyika ni miongoni mwa utekelezaji wa Ilani ya
Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020 ambayo mpaka hivi sasa tayari imeshatekelezwa
kwa kiwango kikubwa.
Pamoja na hayo, Rais
Dk. Shein alisisitiza haja ya kutunza mazingira kwani miongoni mwa sababu za
uhaba wa maji katika Mkoa wa Mjini kunatokana na uharibifu wa mazingira
uliofanywa katika vianzio vya maji zikiwemo chemchem.
Nae Waziri wa Ardhi,
Nyumba, Maji na Nishati Salama Aboud Talib alieleza juhudi zinazochukuliwa
katika kuhakikisha mradi huo unakamilika huku akitumia fursa hiyo kumpongeza
Rais Dk. Shein kwa kutekeleza Ilani ya CCM ya katika kuhakikisha wananchi wa
Mkoa wa Mjini wanapata maji safi na salama.
Mapema Mkurugenzi Mkuu
wa Mamlaka ya Maji Zanzibar Mussa Ramadhani Haji alieleza kuwa alieleza kuwa
Mradi wa Maji na Usafi wa Mazingira wa Mkoa wa Mjini Magharibi (ZUWSP)
unatekelezwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Benki ya
Maendeleo ya Afrika (AfDB) na
utekelezaji wake ulianza mwaka 2013 na unatarajiwa kumalizika mwezi wa Disemba
2019.
Mradi huo unajumuisha
uchimbaji wa visima vipya 6, ukarabati wa visima vikongwe 23, ujenzi wa Matangi
2 yenye ujazo wa lita Milioni mbili 2,000,000 Saateni na Milioni Moja 1,000,000
Mnara wa Mbao, ulazaji wa mabomba makubwa yenye urefu wa kilomita 20 kutoka
Bumbwisudi hadi Welezo matangini pamoja na ulazaji wa mabomba yenye urefu wa
kilomita 60 kutoam Welezo hadi kwa watumiaji.
Aidha, Mkurugenzi huyo
alieleza kuwa Mradi huo hadi kukamilika kwake unatarajiwa kugharimu jumla ya
Dola za Kimarekani Milioni 23 sawa na TZS Bilioni 37.1 ambapo SMZ imetoa TZS Bilioni 3.8 na TZS
Bilioni 33 zitatolewa kwa Mkopo kutoka Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB).
Wakati huo huo, Rais
Dk. Shein ambaye pia, ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar alikutana na wanachama na viongozi wa CCM wa
Mkoa wa Mjini na kufanya nao mazungumzo katika ukumbi wa CCM Mkoa wa Mjini
uliopo Amani ambapo katika mazungumzo yake alisisitiza suala zima la umoja na
mshikamano.
Aidha, Rais Dk. Shein
amewasisitiza wanaCCM pamoja na viongozi wa Chama hicho kuweka mazingira mazuri
ya kushinda uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2020 kwa kufanya maandalizi mazuri.
Alisisitiza kuwa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzbar imekuwa ikitekeleza mambo yote yaliyomo kwenye
Ilani ya Uchaguzi na yale ambayo hayamo kwenye Ilani hiyo lakini kutokana na umuhimu
wake imekwua ikiyatekeleza kwa kiwango cha hali ya juu na kulea mfano ujenzi wa
barabara katika eneo la Mwanakwereke, Kibondemzungu pamoja na ujenzi wa mitaro
ya maji machafu katika mji wa Zanzibar.
Sambamba na hayo, Rais
Dk. Shein aliwataka wanaCCM kuwaepuka waongo ambao wamekuwa wakizusha mambo
mbali mbali ambayo hayana msingi ikiwa ni pamoja na kuzua kuwa yeye na Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Joseph Magufuli wana mpango wa kufanya kuwepo
na Serikali moja tu ambayo ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Rajab
Mkasaba, Ikulu
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment