Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, Awaapisha Viongozi Aliowateua Hivi Karibuni.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimuapisha Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Mhe. Balozi Mohammed Ramnia Abduwawa, kabla ya uteuzi huo alikuwa Mshauri wa Rais Masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa Fedha na Uchumi. Hafla hiyo imefanyika leo Ikulu Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein leo amewaapisha viongozi aliowateua hapo jana kushika nyadhifa mbali mbali katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Viongozi walioapishwa na Rais Dk. Shein katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar ni Balozi Mohamed Ramia Abdiwawa, anaekuwa Waziri wa Fedha na Mipango, Haroun Ali Suleiman anaekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Wengine ni , Mmanga Mjengo Mjawiri,Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi, Khamis Juma Mwalimu anaekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Simai Mohammed Said ambaye anakuwa Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali

Viongozi wengine walioapishwa ni Yakout Hassan Yakout anaekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Joseph Kazi  anaekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria na Dk. Omar Ali Ameir anaekuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia masuala ya Mifugo na Uvuvi.

Aidha, Rais Dk. Shein amemuapisha, Seif Shaaban Mwinyi  anaekuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Salhina Ameir Mwita anaekuwa Naibu Katibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati pamoja na Mansura Mosi Kassim anaekwua Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kilimo na Maliasili.

Hafla hiyo, ilihudhuriwa na viongozi mbali mbali akiwemo Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd,  Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee.

Viongozi wengine waliohudhuria hafla hiyo ni Mawaziri, Manaibu Mawaziri, Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabih, Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman Ngwali pamoja na Sheikh Mahmoud Mussa Wadi, Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar.

Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib, Washauri wa Rais wa Zanzibar, Wakuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama pamoja na viongozi wengine wa Serikali.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.