Habari za Punde

 
Baadhi ya Watoto wanaoishi katika Nyumba ya Watoto Yatima ya Serikali Mazizini Zanzibar, wakipata futari maalum walioandaliwa na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, iliofanyika katika makazi yao na kuungana pamoja katika hafla hiyo.  
Watoto  wa Nyumba ya Watoto Yatrima ya Serikali Mazizini Zanzibar wakipata futari wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika makazi yao Mazizini Zanzibar.
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi, wakijumuika na Watoto wa Nyumba ya Serikali Mazizini katika futari maalum aliyowaandalia na kujumuika nao katika makazi yao Mazizini Zanzibar.jana 28-5-2019
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akijumuika katika futari maalum aliyowaandalia Watoto wa Nyumba ya Watoto Yatima Mazizini Zanzibar, kulia Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi na kushoto Waziri wa Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto Zanzibar Mhe. Maudline Castico, wakishiriki katika hafla hiyo ya futari katika makazi ya Watoto Mazizini Zanzibar. 

   












No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.