Na
Raya Hamad (WKS)
Imeelezwa kuwa azma ya Serikali
ya Mapinduzi Zanzibar ni kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma stahiki za
msaada wa sheria kutoka kwa wanasheria ambao
wana sifa zinazohitajika kwa mujibu
wa sharia.
Mkurugenzi wa Idara ya Msaada wa
Kisheria Bi Hanifa Ramadhan Said
ameyasema hayo wakati alipokuwa akifunguwa mafunzo ya siku moja ya kujenga uelewa kwa wasaidizi watoaji huduma za msaada
wa kisheria kutoka taasisi mbali mbali za watoa huduma kwenye ukumbi wa mkutano
Wizara ya Katiba na Sheria Mazizini.
Bi Hanifa amesema kuwa kila
mwananchi anayo haki ya kupata msaada wa
kisheria bila ya ubaguzi kwa mujibu wa Sheria na Katiba ya Zanzibar ya mwaka
1984 ambayo inasisitiza kulindwa kwa haki za binadamu
“Uwepo wa Idara ya Msaada wa
Kisheria Zanzibar, kunafungua ukurasa mpya katika kuhakikisha kuanzisha haki na
wajibu kwa watoaji wa msaada wa huduma za kisheria, vigezo na viwango pamoja na
usimamizi mzima wa huduma za msaada wa kisheria” alisisitiza.
Mkurugenzi Hanifa ameiomba jamii kuwa tayari kuitumia Idara ya Msaada wa
Kisheria pamoja na wasaidizi wake kwa
utaratibu maalum uliowekwa kwani sio watu wote watapewa huduma hio isipokuwa
kwa yule asie na uwezo kama sheria na kanuni zinavyoelekezwa
Aidha
amesisitiza kuwa Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 inatambua na inahakikisha
haki na inajumuisha suala la msaada wa kisheria kama msingi wa haki za binadamu
kwa watu wote hivyo ni wajibu wa watoaji wa msaada wa kisheria kuifuata
miongozo iliyowekwa ili kuweza kuisaidia jamii kupata msaada wa kisheria kwa
ufanisi na kwa wakati.
Nao
wawezeshaji wa mafunzo hayo na maafisa Sheria kutoka Idara ya msaada ya kisheria Bw Ali Haji
Hassan na Bi Hajar Idrisa Haji wamewataka washiriki hao kufanya tathmini na
kuwa waangalifu pale mdai anapopeleka
maombi yake ikiwemo kutoa
vipaumbele kwa masuala ya watoto, wazee, watu wenye ulemavu,
unyanyasaji wa kijinsia udhalilishaji, migogoro ya ardhi, uriti, huduma za
mtoto na masuala ya uvunjifu wa haki za binaadamu.
Ndugu Ali amesema mtoa huduma
atahitajika kuweka utaratibu wa tathmini ya huduma anayoitoa kwa ufatiliaji wa
mwenendo wa ushauri, mafunzo na taarifa za kila mwezi na kumbukumbu za vikao na
kusisitiza kuwa kanuni imeweka wazi juu na kutoa muongozo kwa watoa huduma hao
Aidha katika kuweka usimamizi
mzuri, kanuni imeweka wazi kuwa msaidizi wa sheria katika utekelezaji wa
majukumu yake atakuwa chini ya uangalizi wa Wakili au Mwanasheria
Bi
Hajar amezianisha baadhi ya kazi tofauti zinazofanywa na Idara ya Msaada wa
Kisheria ikiwemo kutoa miongozo ya kisera kwa watoaji wa msaada wa kisheria, kusajili
watoaji wa msaada wa kisheria, Kumtaka mtoa msaada wa kisheria kutoa huduma ya
msaada wa kisheria kwa mtu asiekuwa na uwezo, na kumshauri Waziri kuhusu sera
na mambo mengine muhimu yanayohusu kuimarisha utaoaji wa msaada wa kisheria.
Katika
kuleta ufanisi na kufanikisha kazi za
utoaji msaada wa huduma za kisheria
kanuni zimeelezea utaratibu maalum kwa watoaji wa msaada huo, ikiwemo
taasisi au mtu anayetoa huduma hizo kuhakikishwa uwezo wake wa kufanikisha kazi
hiyo, ili kuepuka ubabaishaji wakati wa utoaji wa huduma.
Wawezeshaji
hao wamewaomba watoaji wa msaada wa kisheria kuipa mashirikiano ya kutosha
Idara ili kuweza kufikia malengo pia kuzisoma na kuzielewa vizuri kanuni kwa
lengo la kufikisha elimu kwa walengwa ambao ni wataka huduma wa msaada wa
kisheria
Wakitoa
michango yao washiriki wa mafunzo hayo wameomba kuwepo kwa mikutano mara mbili
kwa mwaka kwa wasaidizi wote wa msaada wa kisheria, aidha wameomba kupatiwa
vitambulisho maalum ili watakapokwenda kwa wananchi waweze kuwafahamu kiraisi
pamoja na kuwatumia watoa huduma za msaada wa
kisheria kwa wasomi wa vyuo vikuu vilivyopo nchini.
No comments:
Post a Comment