Mkuu wa Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro Bw.
Adam Mgoi akizungumza Wilayani Bahi mkoani Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe.
Selemani Jafo wakati wa hafla ya uzinduzi na usambazaji wa taarifa ya kutenga maeneo ya kuhesabia watu kwa ajili ya Sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika mwaka
2022
Na
Mwandishi Wetu- Dodomass.
Serikali ya Awamu
ya Tano imedhamiria kuboresha maisha ya wananchi kwa kutumia takwimu
zinazokusanywa ili kuwezesha kupangwa kwa mipango ya maendeleo inayoendana na
mahitaji ya wananchi katika huduma za jamii.
Akizungumza Oktoba
17, 2019 huko Bahi mkoani Dodoma wakati wa uzinduzi na usambazaji wa taarifa ya
kutenga maeneo ya kuhesabia watu ya Wilaya ya Bahi, Waziri wa Nchi Ofisi ya
Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo alisema kuwa
taarifa zinazotokana na takwimu zitasaidia katika upangaji wa mipango
unaoendana na mahitaji ya wakati.
Katika hotuba yake
iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Bw. Adam Mgoi, Waziri
Jafo alieleza ili kutekeleza dhamira ya serikali ya kuwatumikia vyema wananchi ni
lazima kufahamu idadi
ya wananchi wake, hali zao za kiuchumi, mahali walipo, elimu yao, afya zao na
mahitaji yao ya msingi.
Aliueleza mkutano huo kuwa
Takwimu zinazokusanywa wakati wa Sensa ni nyenzo muhimu kwa utayarishaji wa
sera za kiuchumi na maendeleo, na inatumika katika kuangalia uboreshaji wa hali
ya maisha ya watu.
Alipongeza Ofisi ya Taifa
ya Takwimu na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar kwa kufanya kazi kwa
weledi na ikiwemo kufanya maandalizi ya Sensa ya Watu na Makazi miaka mitatu
kabla ya zoezi la kuhesabu watu kufanyika kama miongozo ya kimataifa
inavyoelekeza.
“Mataifa mengi ya
Afrika yanakuja kujifunza hapa Tanzania jinsi Ofisi ya Taifa ya Takwimu
inavyotekeleza majukumu yake kwa ufanisi hali iliyowezesha hata kuanza kwa
zoezi hili la utengaji wa maeneo ya kuhesabia watu kwa ajili yan Sensa ya watu
na makazi ya mwaka 2022” Alisisitiza Mgoi
Akifafanua amesema
kuwa viongozi Viongozi katika ngazi zote hapa nchini wanapaswa kutoa
ushirikiano kwa watafiti kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu wakapokuwa
wakitekeleza jukumu la utengaji wa maeneo ya kuhesabia watu ikiwa ni maandalizi
ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 itakayofanyika hapa nchini.
Aliongeza kuwa Sensa
hiyo inatarajiwa kufanyika kwa kutumia mifumo ya kisasa ya TEHAMA na hivyo
kupunguza gharama kuanzia katika hatua za utengaji wa maeneo hadi utekelezaji
wa zoezi la sensa mwaka 2022.
Kwa upande wake Mtakwimu
Mkuu wa Serikali Dkt Albina Chuwa aliishukuru Serikali na wadau wa maendeleo
kwa kuendelea kuwezesha utekelezaji wa majukumu yake kwa ufanisi ikiwemo kuanza
kwa zoezi la kutenga maeneo ya kuhesabia watu kwa ajili ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022.
Aliongeza kuwa
Ofisi yake inapata ushirikiano wakutosha katika mamlaka za Serikali za Mitaa
hali inayowezesha kutekelezwa kwa ufanisi kwa zoezi hilo katika Wilaya ya Bahi,
Kondoa na Chamwino ambapo kwa Bahi tayari limekamilka pamoja na Sehemu ya
Wilaya ya Kondoa.
Naye Mwakilishi wa
Benki ya Dunia Bi Elizabeth Talbert amesema kuwa wataendelea kusaidia juhudi za
Serikali katika kufanikisha Sensa ya mwaka 2022 ili kuchochea maendeleo kwa kuwa
Benki hiyo hutumia takwimu hizo katika kusaidia miradi ya maendeleo.
Zoezi la kutenga
maeneo ya kuhesabia watu kwa ajili ya Sensa
ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 mkoani Dodoma limekamilika katika Wilaya za
Bahi na Chamwino pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa Vijijini na hivi
sasa linaendelea katika Halmashauri ya Kondoa mjini.
Kwa kawaida, Sensa
ya Watu na Makazi hufanyika kila baada ya miaka kumi. Sensa ya mwisho kufanyika
humu nchini ilikuwa mwaka 2012.
MtakwimumkuuwaSerikalikutokaOfisiyaTaifayaTakwimu
(NBS) Dkt.
AlbinaChuwaakielezafaidazakutengamaeneoyakuhesabiawatukwakutumiamfumowakidigitalikwaajiliyaSensayawatunamakaziinayotarajiwakufanyikamwaka
2022
wakatiwahaflayauzinduzinausambazajiwataarifayakutengamaeneohayoiliyofanyikaWilayaniBahimkoani
Dodoma.
MkuuwaWilayayaBahiMhe.
MwanahamisMunkundaakizungumzaJafowakatiwahaflayauzinduzinausambazajiwataarifayakutengamaeneoyakuhesabiawatukwaajiliyaSensayawatunamakaziinayotarajiwakufanyikamwaka
2022.
Mwakilishi
waShirika la UmojawaMataifalinaloshughulikiaIdadiyaWatuBw. Wilfred
OchanakielezakuhusumikakatiyaShirikahilokuungamkonomikakatiyaSerikalikufanikishaSensayawatunamakaziinayotarajiwakufanyikamwaka
2022.
Mwakilishi kutokaBenkiyaDunia Bi. Elizabeth Talbert
akizugumziaumuhimuwa sense
nazoeziyakutengamaeneoyakuhesabiawatukwaajiliyaSensayawatunamakaziinayotarajiwakufanyikamwaka
2022.
MkuuwaWilayayaKilosamkoaniMorogoroBw.
Adam MgoiakikatautepekwaniabayaWaziriwanchi, OfisiyaRais,TawalazaMikoanaSerikalizaMitaa
(TAMISEMI) Mhe. SelemaniJafokuzinduataarifayaWilayaniBahimkoani Dodoma baadayakukamilikakwazoezizakutengamaeneoyakuhesabiawatukwaajiliyasensayawatunamakaziyamwaka
2022 ,haflahiyoiliyofanyikaOktoba 17, 2019.
No comments:
Post a Comment