Taarifa
kwa Vyombo vya Habari
Dar
es Salaam. November 1st, 2019. Kampuni ya simu za mkononi Zanzibar Telecom Public Limited
Company (Zantel), leo, imetangaza kukamilika kwa mchakato wa kuungana na
kampuni ya MIC Tanzania Public Limited Company (Tigo). Hii ni baada ya kupokea
idhini kutoka mamlaka husika na sasa kampuni hizi mbili zinaungana na kuwa
kampuni moja Tanzania Bara na Visiwani.
Akizungumzia
juu ya suala hilo, Brian Karokola, Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Zantel, alisisitiza kwamba kampuni zote
mbili zinakuja pamoja kwa lengo la kushirkiana na serikali kusogeza mbele
maendeleo ya Tanzania: "Kupitia utoaji wa huduma bora kwa wateja, intaneti
yenye kasi kubwa, mchanganyiko wa bidhaa zenye ubunifu wa hali ya juu na kuenea
kwa huduma katika sehemu kubwa ya nchi, muunganiko wa kampuni hizi utaimarisha ushindani katika sekta ya mawasiliano ya simu kwa faida
ya nchi kwa ujumla. Hakika hii ni habari njema kwa wateja wa Zantel ambao
wataweza kupata huduma za hali ya juu za Tigo na kufaidika na bidhaa na huduma
za kisasa na za hali ya juu."
Kuunganishwa
kwa biashara hizi, kutaongeza nguvu kwenye makampuni haya mawili ya Zantel na
Tigo katika kuhudumia vyema na kwa ubora zaidi wateja wetu walioko Zanzibar na
Bara. Vilevile wateja watapata mawasiliano mazuri zaidi maeneo yote ya mijini
na vijijini na kuwezesha pia upatikanaji wa suluhisho la mawasiliano kwa
biashara mbalimbali pamoja na huduma za kifedha kupitia simu za mkononi kwa
wateja wa Zantel na Tigo.
Uongozi
wa Zantel na Tigo utahakikisha kuwa mchakato wa kuunganisha uendeshaji wa
kampuni hizo mbili utawezesha wateja kuendelea kufurahia huduma zote za
mitandao
yao
husika yani Zantel na Tigo bila matatizo yoyote. Namba na taarifa za wateja hazitabadilika
na hakutakuwa na usumbufu katika upatiknaji wa mawasiliano, huduma na bidhaa
wakati wote wa zoezi la kuunganishwa kwa kampuni hizi mbili.
//ENDS//
Kwa
taarifa zaidi wasiliana na:
Rukia Mtingwa – Senior Specialist PR,
CSR & Media
Mobile: +255 774 55 9999
No comments:
Post a Comment