Habari za Punde

Mashindano ya Akina Mama Kumekucha 2019 Yawa Kivutio Mjini Musoma.

Mwenyekiti wa UWT Taifa Mama Gaudesia Kabaka akizungumza wakati akifungua Mashindano ya Wakina mama yaliyopewa jina la Kumekucha akina mama wa Musoma 2019

Na.Mwandishi Wetu - MUSOMA


MASHINDANO ya Wakina mama yaliyopewa jina la Kumekucha akina mama wa Musoma 2019 yamekuwa kivutia kukibwa Musoma Mjini huku waaandaji wakihaidi kuendelea
kuyafanya kila mwaka lengo kutoa fursa kwa wanawake kuonyesha vipaji vyao kupitia huko.

Mgeni rasmi kwenye mashindano hayo alikuwa Mama Gaudesia Kabaka Mwenyekiti wa UWT Taifa ambapo alipongeza waandaaji wa mashindano hayo na kusema  hii ni mara ya kwanza kwa mashindano hayo kutokea Mara Kwani haijawahi kutokea na yameendeshwa kwa kufuata kanuni za mashindano kwa michezo.

Michezo ambayo ilifanyika kwenye mashindano hayo ni Netball, wakina mama kukimbiza kuku, kuvuta kamba na kukimbiza magunia ikiwa ni mkakati wa kuhakikisha tunaendelea vipaji vya wakina mama.

Mashindano hayo yaliandaliwa na Mlezi wa Chama cha mchezo wa Netball Mkoani Musoma mjini Wakili Suzana Senso alisema kwamba wameamua kuandaa mashindano hayo kwa sababu wakina  mama wanakuwa wamesahaulika kwenye michezo hasa Netball.

Akizungumza wakati wa mashindano hayo Mlezi wa Chama cha Mchezo wa Netball mkoani Musoma Wakili Suzana alisema kwamba alisema wameamua kuanzisha mashindano hayo ili kutoa fursa kwa wakina mama nao kuweza kuonyesha vipaji vyao walivyonavyo.

“Kikubwa zaidi niwaambie kwamba tumeamua kufanya mashindano hayo kwa wakina mama waweze kuonyesha vipaji vyao kwani mabonanza mengi hayausishi wakina mama hilo ndilo ambalo limewasukuma kuwasiliana na Naibu Meya wa Musoma Mjini Bwana Igwe na tukaona tuandae hicho kitu tunamshukuru Mungu kimekwenda vizuri”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba pia wana mpango wa kuandaa mashindano mengine ya wakina mama yatakayofanyika Machi 8 mwakani lengo kubwa ni kuhakikisha wanawawezesha kushiriki kwenye mashindano mbalimbali nao waweze kuendeleza vipaji vyao.

Hata hivyo aliyashukuru makampuni mbalimbali yaliyojitokeza kuunga mkono mashindano hayo kwa kuyasaidia ambao ni Uhuru Hospitali, Chama cha Netbally Mkoa Musoma na Meya wa Manispaa Musoma, UWT Mkoa.

Naye kwa upande wake Mkurugenzi wa Uhuru Hospitali Dkt Derick Nyasebwa alisema kwamba wameamua kushiriki mashindano hayo ya wakina mama na wamefurahi kwa sababu yeye pia ni mzaliwa lakini kwa niaba ya Uhuru Hospitali .

Alisema waliamua kuhakikisha wanashiriki kwenye michezo  hiyo kwani kufanya hivyo ni kampeni kubwa zinazoendelea nchini kutoka wizara ya Afya,maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto inayoongozwa na  Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kuhakikisha wanaelimisha watu kuepukana na magonjwa yasiyoambuliza kupitia michezo ni njia nzuri ya kuepukana na kusukari,saratani na msukumo wa damu kuwa juu.
Mlezi wa Chama cha mchezo wa Netball Mkoani Musoma mjini Wakili Suzana Senso ambaye pia ni Mdhamini wa Mashindano hayo akizungumza wakati wa ufunguzi
Mwenyekiti wa UWT Taifa Mama Gaudesia Kabaka kulia akifuatilia mashindano hayo kushoto ni Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Mara Wegesa Hassan
Mlezi wa Chama cha mchezo wa Netball Mkoani Musoma mjini Wakili Suzana Senso ambaye pia ni Mdhamini akifuatilia mashindano hayo ambaye pia ni miongoni mwa waandaaji wa mashindano hayo akifuatilia kwa umakini
Wadhamini wakiwa na washindi wa kwanza kutoka kushoto watatu ni Naibu Meya wa  Musoma mjini Mr. Igwe  na wanne kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Uhuru Hospitali  Derick Nyasebwa
moja kati ya mechi zikiendelea uwanjani
Mlezi wa Chama cha mchezo wa Netball Mkoani Musoma mjini Wakili Suzana Senso ambaye pia ni Mdhamini katikati akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya timu zinazoshiriki mashindano hayo
Mwenyekiti wa UWT Taifa Mama Gaudesia Kabaka katikati akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wadau wa michezo mjini Musoma wa pili kulia ni Mlezi wa Chama cha mchezo wa Netball Mkoani Musoma mjini Wakili Suzana Senso ambaye pia ni Mdhamini mashindano hayo kushoto ni Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Mara Wegesa Hassan
Kamati ya maandalizi ikiongozwa na Mwenyekiti wa netball Musoma mjini Bi Godviler

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.