Uongozi wa masjid ikhlasw uliopo shaurimoyo
Zanzibar tayari umepanga kuleta maombi kwenu
waislamu kwa lengo la kupanua msikiti pamoja na
madrasa (chuo) kwa lengo la kuendesha dini ya Allah (s.w) mbele.
Hatua hii ya kupatiwa jengo la msikiti pamoja na
chuo itapelekea kuweza kupata nafasi nzuri ili tuweze kuwasomesha watoto wetu,
watu wazima, pamoja na jamii kwa ujumla, kama alivosema Allah (s.w)... “na
toeni vile alivokupeni m/mungu kabla hayajamfika mmoja wenu mauti……. Suratu-
almunafiqoon. “10”
Kwa kuzingatia hilo basi tunawaomba waislamu wote
hususan wale ambao allah kawajaalia kuwa na mali waitumie fursa hii kwani
kujenga msikiti ni moja kati ya alama kubwa sana ambazo Allah amezisifia, kama
alivosema Allah (s.w)
“hakika sivyenginevyo isipokuwa wale wenye kusimamia Misikiti ya Allah ni wale waliomuamini Allah
na siku ya mwisho” Attauba “18”
Na akasema tena mtume Muhammad (s.a.w) ….
“mwenye kujenga msikiti
mmoja hapa duniani Allah atamjengea nyumba peponi”
Tunategemea maombi yetu haya yatakuwa ni yenye
kuzingatiwa na kufanyiwa kazi.
Tunamuomba Allah atufanyie wepesi juu ya jambo
hili.
MASJID IKHLASW
PBZ A/C NO 0738694001
M'PESA A/C NO 0747656537
TIGO PESA A/C NO 0672519303
WABILAH TAUFIQ
No comments:
Post a Comment