Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt.
Leonard Akwilapo, aliyekuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 55 ya Taasisi ya
Elimu ya Watu Wazima (TEWW) akimpongeza mhitimu aliyekuwa na mahitaji maalum
aliyefanikiwa kuhitimu na kufaulu vizuri licha ya kuwa na ulemavu wa kuona
katika mahafali yaliyofanyika 06.12.2019 Jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Dkt. Michael
Ng’umbi akizungumza wa wahitimu (hawapo pichani) wakati wa Mahafali ya 55 ya
Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima, yaliyofanyika tarehe 06.12.2019 jijini Dar es
Salaam
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia , Dkt. Leonard Akwilapo ( wa
tatu kushoto waliokaa), akifuatiwa na Mwenyekiti wa Baraza la Usimamizi wa
Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) Dkt. Naomi Katunzi , Mkurugenzi wa
Taasisi ya Elimu ya watu Wazima (TEWW), Dkt. Michael Ng’umbi (wa tatu kulia
waliokaa) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wakufunzi wa TEWW
walioshiriki kwenye Mahafali ya 55 ya TEWW yaliyofanyika Jijini Dar es Salaaam
Na
Mwandishiwetu
Wanafunzi 912
wahitimu masomo yao katika Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) kwa mwaka wa masomo
2018/2019.
Akizungumza wakati wa mahafali ya Taasisi hiyo yaliyofanyika Jijini
Dar es Salaam, Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia,Dkt. Leonard
Akwilapo ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo amesema kuwa kati ya wanafunzi hao
138 ni wa shahada, 724 ni stashahada na 50 ni wa stashahada.
“Idadi ya wahitimu kwa mwaka 2018/2019 ni sawa na ongezeko la asilimia 32%
ikilinganishwa na 690 kwa mwaka 2017/2018”; Alisisitiza Dkt. Akwilapo
Akifafanua amesema wahitimu hao wanatoka katika Kampasiza ya Dar es Salaam, wamo kutoka Morogoro na Luchelele Jijini Mwanza wanawake wakiwa 565 na wanaume 397.
Pia Dkt.
Akwilapo amewaasa wahitimu hao kuzingatia weledi na taaluma waliyopata katika kuchangia maendeleo ya Taifa kwa kufuata sheria kanuni na taratibu zilizopo kwa maslahi ya Taifa.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Baraza la Usimamizi
wa Taasisi hiyo Dkt.Naomi
Katunzi amesema kuwa udahili wa wanafunzi umeongezeka kutoka wanafunzi 4,598
katika mwaka wa masomo 2018/2019 na kufikia wanafunzi 7,042 ikiwa ni sawa na ongezeko la
asilimia 75.
Aliongeza kuwa ongezeko hilo litachangia kuongeza mapato ya ndani ya Taasisi hiyo yatakayosaidia katika shughuli za uendeshaji na kuongeza tija.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Michael
Ng’umbi amesema kuwa wamekuwa wakishirikiana na wadau wa maendeleo kutekeleza programu iliyojikita katika kujenga stadi za kusoma,
kuandika na kuhesabu (KKK), Pamoja na stadi za maisha ya ujasiriamali ambapo wanufaika
961 wamefikiwa na mradi huo.
Vilevile wasichana 627 wamenufaika na mradi wa elimu ya Sekondari kwa wasichana walio nje ya shule katika mkoa wa Tanga ikiwa ni sehemu ya juhudi za TEWW kuchangia katika kukuza kiwango cha elimu hapa nchini na kupunguza idadi ya wanaokosa fursa ya elimu kwa sababu mbali mbali ikiwemo mimba za utotoni.
Aidha, Dkt.
Ng’umbi amesema kuwa TEWW inajukumu la kushirikiana na wadau binafsi kuwapatia elimu watoto,
na vijana takribani milioni 3.5 waliokatisha masomo kwa sababu za utoro na mimba ili waweze kutoa mchango katika kukuza uchumi kupitia shughuli za uzalishaji.
Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) imekuwa ikishirikiana na wadau kama UNESCO na KOICA kutekeleza miradi mbali mbali inayolenga kukuza kiwango cha elimu na kuyawezesha makundi maalum kama wasichana walikosa elimu katika mfumo rasmi kwa sababu mbalimbali.
No comments:
Post a Comment