Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akizungumzia namna ya kufanya kazi kwa ushirikiano katika masuala ya utawala bora na Makamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora waliomtembelea ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma.
Na Happiness Shayo - Dodoma. 24.01.2020
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) amekutana
na Makamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kwa lengo la
kujadiliana namna ya kufanya kazi kwa ushirikiano hasa katika masuala ya
utawala bora ili kuboresha utendaji kazi na kutoa huduma bora kwa wananchi.
Akizungumza katika kikao kazi hicho kilichofanyika ofisini
kwake Mtumba, jijini Dodoma leo, Mhe. Mkuchika amesema ofisi yake iko tayari
kushirikiana na Tume hiyo kwani ni wajibu na pia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amekuwa akisisitiza kushirikiana kwa
pamoja kabla ya kupeleka hoja mezani kwake.
Aidha, Mhe. Mkuchika amesema kuwa idadi
ya malalamiko ya wananchi yanayofanyiwa kazi na ofisi yake yanaongezeka kila
mwaka kutokana na utandawazi, kuwapo kwa uwazi serikalini na kutolewa kwa elimu
juu ya umuhimu wa wananchi kudai haki zao za msingi.
Mhe. Mkuchika ameweka bayana kuwa ofisi
yake inashughulikia masuala ya utawala bora katika sekta zote hivyo malalamiko
yote akitolea mfano wa sekta ya maji, madini n.k. yamekuwa yakiwasilishwa
ofisini kwake.
Naye, Mwenyekiti wa Tume ya Haki za
Binadamu za Utawala Bora, Jaji (Mst.)
Mathew Mwaimu amesema kuwa lengo la ziara hiyo ni kuomba ushirikiano wa
utendaji kazi kati ya ofisi yake na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora kwa sababu kwa pamoja ofisi hizo zinashughulikia masuala ya utawala bora.
Akizungumzia majukumu ya Tume hiyo, Jaji
(Mst.) Mathew Mwaimu amesema kuwa,
ofisi yake imekuwa ikipokea malalamiko katika eneo la haki za binadamu,
ukiukwaji wa misingi ya utawala bora na malalamiko yanayohusu sekta nyinginezo
kutoka kwa wananchi, hivyo imekuwa ikiwasaidia walalamikaji kutatua changamoto
zinazowakabili kwa kuwasiliana na taasisi husika.
Jaji (Mst.) Mathew amesema kuwa pamoja na changamoto mbalimbali
inazokumbana nazo katika utekelezaji wa majukumu yake, ofisi yake itaendelea
kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha kunakuwa na matokeo chanya katika
kuwahudumia wananchi.
Kikao hicho kimehudhuriwa na Makamishna
wa Tume ya Haki za Binadamu za Utawala Bora na baadhi ya Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, ikiwa ni sehemu ya kufahamiana na kuboresha utendaji kazi wa ofisi hizo.
Kaimu Katibu Mtendaji, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Bi. Fatuma Muya akitoa maoni yake wakati wa kikao kazi cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) na Makamishna wa Tume hiyo kilichofanyika ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma leo kilichokuwa na lengo la kujadiliana namna ya kufanya kazi kwa ushirikiano katika masuala ya utawala bora.
Baadhi ya Makamishna na Viongozi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) wakati wa kikao kilichofanyika ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma leo kuzungumzia namna ya kufanya kazi kwa ushirikiano katika masuala ya utawala bora.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) (wa tatu kutoka kushoto mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Makamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora na baadhi ya watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora mara baada ya kikao kilichofanyika ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma leo kilichokuwa na lengo la kujadiliana namna ya kufanya kazi kwa ushirikiano katika masuala ya utawala bora.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akiagana na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Bw. Mohamed Hamad baada ya kikao na Makamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kilichofanyika ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma leo. Kikao hicho kilikuwa na lengo la kujadiliana namna ya kufanya kazi kwa ushirikiano katika masuala ya utawala bora.
No comments:
Post a Comment