Uongozi wa Masjid Ikhlasw uliopo Shaurimoyo Zanzibar
tayari umepanga kuleta maombi kwenu waislamu kwa lengo la kupanua msikiti pamoja na Madrasa (Chuo)
kwa lengo la kuendesha Dini ya Allah (S.W) mbele.
Hatua hii ya kupatiwa jengo la
msikiti pamoja na chuo itapelekea kuweza kupata nafasi nzuri ili tuweze kuwasomesha watoto wetu,
watu wazima, pamoja na jamii kwa ujumla, kama alivyosema Allah (S.W)... “na toeni vile
alivokupeni Mwenyenzi Mungu kabla hayajamfika mmoja wenu mauti……. Suratu- almunafiqoon. “10”
Kwa kuzingatia hilo basi tunawaomba waislamu wote hususan
wale
ambao Allah kawajaalia kuwa na mali waitumie fursa hii kwani kujenga msikiti ni moja kati ya alama kubwa sana ambazo
Allah amezisifia, kama alivyosema Allah (S.W)
“hakika si vyenginevyo isipokuwa wale wenye kusimamia Misikiti ya Allah ni wale waliomuamini Allah
na siku ya mwisho” Attauba “18”
Na akasema tena Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wasallam
“mwenye kujenga msikiti mmoja hapa duniani
Allah atamjengea nyumba peponi”
Tunategemea maombi yetu haya yatakuwa ni yenye kuzingatiwa na kufanyiwa kazi.
Tuna muomba Allah atufanyie wepesi juu ya jambo hili.
MASJID IKHLASW
PBZ A/C NO 0738694001
M'PESA A/C NO 0747656537
TIGO PESA A/C NO 0672519303
WABILAH TAUFIQ
No comments:
Post a Comment