Habari za Punde

Daktari Li Wenliang Apoteza Maisha Baada ya Kupata Maambukizi ya Virusi Vya Corona

Daktari raia wa China aliyejaribu kutoa tahadhari kuhusu mlipuko wa virusi vya corona amefariki, hospitali iliyokuwa ikimpatia matibabu imeeleza.
Li Wenliang alipata maambukizi wakati akifanya kazi katika hospitali mjini Wuhan.
Alituma ujumbe wa tahadhari kwa madaktari wenzake tarehe 30 mwezi Desemba lakini polisi walimuamuru kuacha ''kutoa taarifa na maoni ya uongo''.
Kulikuwa na ripoti za kukanganya kuhusu kifo chake, lakini inadaiwa na vyombo vya habari kuwa alifariki usiku wa kuamkia Ijumaa.
Virusi vimeua watu 636 na watu 31,161 wana maambukizi nchini China, tume ya taifa ya afya ilieleza kwenye takwimu zake za hivi karibuni.
Vifo hivyo vinahusisha 73 walioripotiwa siku ya Alhamisi.

Ilikuwaje kwa Li Wenliang?

Dokta Li, aliweka habari kwenye mtandao wa Weibo akiwa kitandani hospitalini mwezi mmoja baada ya kutuma ujumbe wa tahadhari.
Daktari huyo mwenye miaka 34 aligundua visa saba vya maambukizi ya virusi ambavyo alifikiri kuwa vilifananana Sars- mlipuko uliowahi kutokea mwaka 2003.
Tarehe 30 mwezi Desemba alituma ujumbe kwa madaktari wenzake akiwatahadharisha kuvaa vifaa vya kujikinga kuepuka maambukizi.
Siku nne baadae aliitwa na idara ya usalamaambapo aliamriwa kusaini barua. Katika barua hiyo alikuwa akishutumiwa ''kutoa taarifa za uongo'' ambazo zimeleta taharuki miongoni mwa jamii''.
Alikuwa mmoja kati ya watu nane ambao polisi walisema walikuwa wakichunguzwa kwa makosa ya ''kueneza uzushi'' mamlaka baadae zilimuomba radhi Dokta Li.
Katika taarifa aliyoiweka kwenye mtandao wa Weibo alieleza namna alivyoanza kukohoa mwezi Januari, siku iliyofuata alipata homa na siku mbili baadae alikuwa hospitalini. Aligundulika na virusi vya Corona tarehe 30 mwezi Januari.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.