Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Rufaa (Mst.) Semistocles Kaijage akisoma hotuba ya ufunguzi wa Mkutano wa Wadau, Jijini Dar es Salaam
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) leo imefanya vikao na wadau wa Uchaguzi
wa mikoa ya Dar es Salaam na Pwani ikiwa ni maandalizi ya Uboreshaji wa
Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. Uboreshaji wa Daftari kwenye mikoa hiyo
utafanyika kwa siku saba (7) kuanzia tarehe 14 hadi 20 Februari 2020.
Mikutano hiyo ilifunguliwa na kuongozwa na Mwenyekiti wa Tume, Mhe. Jaji
Rufaa (Mst.) Semistocles Kaijage kwa Dar es Salaam na Makamu Mwenyekiti wa
Tume, Mhe. Jaji Rufaa (Mst.) Mbarouk Salim Mbarouk kwa mkoa wa Pwani.
Mikutano hiyo imewakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo Viongozi wa
Vyama vya Siasa,Viongozi wa Dini, Wawakilishi wa Asasi za Kiraia,
Wawakilishi wa makundi maalum ya Watu wenye Ulemavu, Vijana na
Wanawake, Wanahabari na Wazee wa Kimila.
Viongozi hao wa Tume wamewaasa wadau hao kushirikiana na Tume
kuwahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na kuboresha
taarifa zao kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
Kwa upande wake Mhe.
Jaji Rufaa (Mst.) Mbarouk Salim Mbarouk ametoa rai kwa wananchi wa Kata ya
Kibuta wilayani Kisarawe ambao walishiriki kwenye zoezi la uboreshaji wa
majaribio kujitokeza kwa wingi ili taarifa zao ziweze kuingizwa rasmi kwenye
Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. 2
Uboreshaji huu unawahusu Raia wa Tanzania ambao wametimiza umri wa
miaka 18 na wale ambao watatimiza umri wa miaka 18 siku ya Uchaguzi Mkuu
mwezi Oktoba (2020). Pia, unawahusu wale ambao wamehama kutoka maeneo
yao ya awali na kuhamia maeneo mengine ya Uchaguzi na wale ambao Kadi zao
zimeharibika au kupotea.
Zoezi la uboreshaji litahusisha kuondolewa kwenye
Daftari la Kudumu la Wapiga Kura wale waliofariki na wengine waliopoteza
sifa.
Kwa mujibu wa Kifungu cha 15(5) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi,
Sura ya 343 na kifungu cha 21(5) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali
za Mitaa Sura ya 292, Tume inapaswa kuboresha Daftari la Kudumu
la Wapiga Kura mara mbili kati ya Uchaguzi Mkuu mmoja na
Uchaguzi Mkuu unaofuatia.
“Kadi yako, Kura yako. Nenda Kajiandikishe”
Imetolewa na:
Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura
No comments:
Post a Comment