Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia katika hafla ya Maadhimisho ya Siku ya Sheria Zanzibar yaliofanyika katika Ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakiul Kikwajuni Jijini Zanzibar.leo 11,Febuary 2020.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali
Mohamed Shein amewataka wananchi kuheshimu kazi, majukumu na maamuzi ya Tume za
Uchaguzi nchini, kwa kuzingatia kuwa taasisi hizo zimeundwa kwa mujibu sheria
na Katiba za nchi.
Dk. Shein amesema hayo katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdul
wakil Kikwajuni mjini hapa katika kilele cha maadhimisho ya siku ya sheria
Zanzibar.
Alisema kila mwananchi ana wajibu wa kuhakikisha anaheshimu
kazi za vyombo hivyo katika uendeshaji
na utoaji wa maamuzi katika masuala yote yanayohusu uchaguzi wa Zanzibar na ule
wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Alisema wananchi wana wajibu wakuejiepusha na vitendo vyote
vinavyokwenda kinyume na sheria na kanuni zilizowekwa na Tume ya Uchaguzi ya
Zanzibar (ZEC) pamoja na ile ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania (NEC).
Alisema ni vyema kuhakikisha kwamba kila mwenye sifa na haki
ya kushiriki katika uchaguzi huo, anafanya hivyo kwa kuelewa kuwa huo ni msingi
muhimu wa kudumisha utawala bora na Demokrasia.
Aidha, alizitaka taasisi zinazoshughulikia masuala ya uchaguzi
pamoja na usalama wa wananchi kufahamu wajibu walionao na kutekeleza majukumu
yao ipasavyo, akibainisha umuhimu wausalama wanchi kuwa ndio lengo la Serikali.
“Ni vyema ikafahamika kuwa suala la kuendeleza demokrasia na
kudumisha hali ya usalama na amani wakati wote ni wajibu wetu wa kikatiba”,
alisema.
Alisema Zanzibar ina nafasi ya kujifunza njia bora katika
kuendesha kampeni za uchaguzi kwa kuzingatia hoja, ajenda na mambo muhimu ya
maendeleo ya jamii na nchi, kama ilivyobainishwa katika Ilani za Uchaguzi
badala ya kutumia mwanya huo kufanya kampeni zenye kuleta mifarakano, chuki na
uhasama.
Rais Dk. Shein alisema kuna umuhimu wakuhakikisha kampeni za
uchaguzi haziwagawi watu kutokana na rangi zao, makabila yao, dini au miji na
vijiji walivyotoka.
Akigusi kauli mbiu ya maadhimisho hayo isemayo “Dumisha
utawala wa sheria na Demokrasia katika uchaguzi mkuu 2020”, Dk. Shein
alisema suala la kuendeleza Demokrasia
na kudumisha hali ya usalama na amani wakati wote ni wajibu wa kikatiba.
Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetunga sheria ya
uchaguzi namba 4 ya 2018, ikiwa ni juhudi za kukuza na kudunisha demokrasia na
utawala bora pamoja na kuhakikisha uchaguzi unakuwa huru na wa haki.
Alisema sheria zimebainisha taratibu zinazopaswa kuchukuliwa
pale wananchi wasiporidhika na hatua zilizochukuliwa na moja ya taasisi
zinazoshughulikia mchakato wauchaguzi.
“Iwapo mtu hukuridhikana uamuzi wa Tume ya Uchaguzi anaweza
kupeleka shauri lake mahakamani kwauamuzi”, alisema.
Alieleza kuwa uamuzi wowote utakaokwendakinyume na taratibu
zilizowekwa na sheria, zitasababisha zogo na kuanzisha fujo na hivyo kuwa
chanzo cha watu kugombana na hatimae kuingiana maungoni.
Alisema Serikali haitasita kuchukulia hatua za kisheria dhidi ya watu wote watakaobainika kuhusika
na matukio ya aina hiyo.
Alisema kila nchi Duniani ina mfumo wake wa utawala na demokrasia,
sambamba na taratibu zakuendesha uchaguzi, ikiwemo namna ya kuwapata viongozi wakushika nyadhifa tofauti Serikalini.
“Watanzania tuna mfumo wa Demokrasia unaokidhi hali ya usalama
na mazingira yetu na ndio maana sio sahihi na sio halali, si haki na haifai kwa
Taifa jengine kuingilia mfumo na taratibu halali za uchaguzi wanchi yetu
zilizowekwa na Tume ya Uchaguzi”, alisema.
Aidha aliwataka viongozi wavyama vya siasa kuzingatia jukumu
kubwa la kuwatumikia na kuwasimamia wanachama
na wafuasi wao kwa kuzingatia misingi ya demokrasia na utawala bora.
“Si vyema chama cha siasa kushutumu kukosekana kwamisingi ya
demokrasia katika chama kingine na taasisi nyengine wakati hali hiyo ni mbaya
zaidi ndani ya chama kinacholalamika”, alisema.
Dk. Shein alibainisha kuwa demokrasia ya kweli inahitajika
ndani ya uongozi wa vyama vya siasa kwakuweka misingi bora ya kuendesha chaguzi
za viongozi, kutoa fursa za uongozi kwa watu wenye uwezo pamoja na kujiepusha
na hatua za kung’ang’ania madaraka.
Alisema wakati Taifa likijiandaa na uchaguzi mkuu ujao, ana
imani kubwa na vyombo vya sherina kusisitiza umuhimu wa kutekeleza vyema
majukumu yao kwa uadilifu na haki.
Alisema Serikali itaendelea kuhakikisha hali ya amani na
utulivu nchini inaendelea kudumu, na kuwakumbusha wananchi jukumu la kuimarisha
utawala wa sheria pamoja na kulinda usalama.
Akigusia juu ya uhuru wa mahakama, Dk. Shein alisema katika
kipindi chote akiwa madarakani hajawahi wala kuweka azma ya kuingilia uhuru wa
chombo hicho, kwakutambua kuwa ndio nguzo na mhimili wa utawala usiopaswa
kuingiliwa.
Alitoa shukurani kwa watendaji wote wa Mahakama pamoja na wale
waliochangia na kushiriki katika utayarishaji wa toleo la nane la Kitabu cha
“Zanzibar Yearbook of Law”, akibainisha matumaini yake kuwa kitabu hicho
kimetayarishwa baada ya kufanyika utafiti wa kutosha.
Aidha, aliwapongeza watendaji hao kwa ubunifu wao wakuanzisha programu
maalum ya kwenda kwa wananchi, hususan walioko vijijini kwa ajili ya kuwapatia
elimu ya kufahamu haki zao zakikatiba na kisheria.
Mapema, Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omar Othman Makungu alisema sherehe hizo, alisema kwa vipindi tofauti nUchaguzi
wa Zanzibar umekuwa na ushindani mkubwa wakisiasa, hivyo akasisistiza umuhimu wa
jamii kuendelea kulinda amani iliopo.
Alisema mfumo wa Demokrasia ya vyma vingi kamwe haupaswi kuwa
sababu za kuvuruga amani iliopo, akibainisha matukio kadhaa yaliojitokeza katika
chaguzi zilizopita kutokana na wananchi kutotii sheria.
Makungu alitoa ushauri kwa kuwataka wanasheria na mawakili wa kujitegemea
kupelekea mapendekezo yao Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili kusikilizwa
kwakuzingatia kuwa Serikali hii ni sikivu, kabla ya kuwasilisha mahakamani.
Alisema Idara ya Mahakama imejipanga kuleta mabadiliko makubwaya
kiutendaji katika miaka mitano ijayo katika suala zima la utoaji wahuduma
Nae, Waziri wa Katiba na sheria khamis Juma Mwalimu, alitowa
wito kwa wananchi kuendelea kuheshimu na kutii sheria za nchi, kwa kuzingatia
kuwa hakuna mtu yeyote alie juu ya sheria.
Alisema Wizara hiyo itaendelea na jukumu la kusimamia Utawala
wa sheria na upatikanaji wa haki kwawananchi wote.
Aidha, Mwanasheria Mkuu wa serikali ya Zanzibar Said Hassan
Said, alisema wakati wakushereherekea siku ya sheria Zanzibar, kuwa hiyo ni
fursa ya kuwakumbusha wananchi juu ya haki waliyonayo ya kupiga kura kwakuzingatia misingi ya utawala
bora na utawala wa sheria.
Alisema dhana ya Utawala bora na utawala wa sheria ni nguzo
muhimu ya kuifanya Demokrasia ishamiri na kuleta ustawi wajamii pamoja na maendeleo yao.
Alisema kila Mzanaibari anayo haki na uhuru wa kushiriki
katika mchakato wauchaguzi ili kufikia maamuzi yatakayoleta hatma njema ya maisha yake na Taifa na kusisitiza wajibu wa kila
mwananchi mwenye sifa kujiandikisha. .
Alitoa wito kwa wanancho wote kutumia fursaya kuchagua
viongozi kwa kuelewa kuwa fursa hiyo hupatikana kila baada ya miaka mitano.
Vile vile, Mkurugenzi wa Mashtaka Ibrahim Mzee Ibrahim,
alisema Ofisi hiyo ina wajibu wa kuwachukulia hatua zakisheria watu wote na
taasisi zitakazotenda makosa ya uchaguzi, hivyo akasisitiza haja ya taasisi zinazoshughulikia
mchakato wauchaguzi kusimamia vyema majukumu yao.
Katika hafla hiyo iliyohudhuria na Viongozi mbali mbali wa
Serikali na wadau wa sekta ya Sheria, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza
la Mapinduzi, Dk. Ali Moahmed Shein, alizindua kitabu cha ‘Zanzibar YearBook of
Law’ pamoja na kupokea zawadi maalum iliyoandaliwa na Uongozi wa Idara ya
Mahakama Zanzibar.
Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822
E-mail:
abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment