Habari za Punde

Virusi vya corona Afrika: 'Hakuna muda wa kunasua uchumi wa Afrika' dhidi ya corona

Virusi vya corona "havitasababisha maelfu ya vifo pekee" barani Afrika, bali pia huenda vikaathiri pakubwa "uchumi na ustawi wa kijamii", kwa mujibu wa kiongozi mkuu wa Afrika katika Shirika la Afya Duniani, Matshido Moeti.
Kauli yake inatukumbusha kuwa mlipuko wa ugonjwa huu si dharura ya kiafya pekee.
Mwaka mmoja uliopita, ripoti ya Afrika kutoka Benki ya Dunia, iliyoangalizia ukuaji wa uchumi wa mataifa ya jangwa la sahara kwa mwaka 2019 na 2020 kwa kiasi cha 2.8%.
Kushuka huko kwa uchumi, kumeshusha malengo ya taarifa nyingi ambazo zilitegemewa kuongeza uchumi, na sasa bara hili litaanguka kiuchumi kwa kiwango ambacho haijakipitia kwa miaka 25, kwa uchumi kushuka kwa kiwango cha kati ya 2.1% na 5.1%, kutokana na athari zinazotokana na kusambaa kwa mlipuko wa ugonjwa wa Covid-19.
Benki ya dunia inasema athari zinazotokana na ugonjwa wa Covid-19 katika bara hilo zimegawanyika katika sehemu tatu:
  • Biashara zimeathirika na kushindwa kusafirishwa kwa bidhaa
  • Fedha za ufadhili kupungua na hata fedha kutoka nchi za kigeni kupungua
  • Matatizo ya kila siku katika uchumi yanayosababishwa na makatazo mbalimbali na watu kufungiwa
Bei ya mafuta , ingawa imekuwa nafuu kidogo lakini gharama yake iko mbali na kile ambacho serikali ya Nigeria inakihitaji ili kuweza kupanga bajeti yao vizuri au kuifanya Angola kukabiliana na anguko la uchumi ambalo nchi hiyo inakumbana nayo kwa sasa.

  • Mwaka mmoja uliopita bei ya madini ya shaba ilikuwa chini ya dola tatu, lakini sasa imeshuka mpaka $2.20.
Bei ya shaba imeshuka karibu karne sasa, lakini mwezi sasa tangu mlipuko wa virusi vya corona ulivyoweza kuathiri zaidi soko hilo la shaba. Na hali mbaya zaidi kwa wasafirishaji wa bidhaa hiyo Zambia.
Mpaka hivi karibuni sekta ya madini nchini Afrika Kusini na Zimbabwe, haikuweza kuendelea kufanya shughuli zake.
Lakini duniani kote kuna hofu bei ya madini kushuka, ni muda tu haujafika.
Mwaka 2018, kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa mataifa na taasisi za maendeleo za kimataifa, Unctad, FDI kuwa bara hilo lilikuwa na maendeleo mazuri.
Lakini sasa Unctad inasema kuwa corona imesababisha uwekezaji kushuka kwa 15%.
Chanzo cha Habari.BBC.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.