Meneja wa Uhusiano na Mawasiliano wa Zantel, Bi. Rukia Mtingwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa Ofa maalumu ya mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan leo jijini Dar es Salaam. Ofa hiyo mpya itawapa wateja uhuru zaidi wa kuwasiliana pamoja na kupata taarifa muhimu kuhusu kipindi
cha mfungo kama nukuu za Quran, pamoja na jumbe za kuwakumbusha muda wa Swala,
kufturu na mwisho wa kula daku.
Zanzibar.23
Aprili 2020.Kampuni ya Mawasiliano ya Zantel, leo
imezindua ofa maalumu yamwezi mtukufu wa Ramadhan kwa wateja wake ili
kuwawezesha kufanya mawasiliano kwa gharama nafuu pamoja na kupata taarifa mbalimbali
zenye kujenga imani zao katika mwezi huu mtukufu
Ofa hiyo inawapa
wateja uhuru wa kuwasiliana zaidi pamoja na kupata taarifa muhimu kama vile nukuumbalimbali
za Koran takatifu pamoja na jumbe za kuwakumbushamuda wa swala na ujumbe wa
sauti utakaoingia kwenye simu zao kama simu nyakati za iftar na nyakati za daku
Akizindua ofa
hiyo mjini Zanzibar, Mkuu wa Zantel Zanzibar Mohammed Mussaalisema ofa hiyo
itawasaidia waumini wa dini ya kiislamu kuimarisha zaidi mahusiano baina ya
ndugu, jamaa na marafiki katika kipindi hiki cha mfungo.
“Zantel inapenda
kuwatakia waislamu wote mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa Ramadhan. Tunatambua mwezi
huu ni muda muafaka wa kujenga mahusiano mazuri na ndugu, jamaa na marafiki
hivyo ofa hii itahakikisha kwamba wateja wetu wanawasiliana bila mipaka na pia
kuwapa taarifa zitakazosaidia kujiimarisha kiimani ili kufanikisha funga zao,”
alisema Mussa.
Naye, Meneja
bidhaa na huduma wa Zantel, Aneth Muga alisema ofa hiyo itawazawadia wateja
watakaojiunga na vifurushi vilivyoboreshwa zaidi vya siku, wiki na mwezi ambapo
mbali na muda wa maongezi watajipatia nukuu za Koran takatifu pamoja na jumbe za
kuwakumbusha muda wa swala tano.
“Tumeboresha
zaidi vifurushi vyetu ili kuwapa wateja sababu zaidi za kuwasiliana msimu
huu.Kwa wateja watakaojiunga kifurushi cha siku kwa Shilingi 1,000/-
watajipatia dakika 150, SMS 100 pamoja na nukuu moja ya Koran, jumbe tano za
kukumbusha muda wa swala,” alisema Muga.
Vilevile, kwa kifurushi
cha wiki cha Shilingi2,000 mteja atapata dakika 250, SMS 200 huku kifurushi cha
mwezi cha Shilingi 10,000/- atapata dakika 1,250, SMS 500 pamoja na nukuu mbalimbali
za maandiko ya Koran takataifu, jumbeza kuwakumbusha muda wa kufuturu pamojaza
kukumbusha muda wa swala.
Ili kujiunga na
ofa hii mteja wa Zantel apige *149*15# na kuchagua namba 1 ambayo ni Ramadhani
ofa na atajiunga na kifurushi anachohitaji.
No comments:
Post a Comment