Habari za Punde

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli Alivunja Bunge la 11 Jijini Dodoma 16/6/2020.

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli na Viongozi wakuu wa Serikali na Wabunge wa Bunge la 11 wakiwa wamesimama wakati ukipingwa wimbo wa Taifa  kabla ya kuaza kwa hafla hiyo Jijini Dodoma. 
WABUNGE wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wakiwa wamesimama wakati ukipigwa Wimbo wa Taifa kabla ya kuaza kwa hafla hiyo  ya uvunjaji wa Bunge la 11,uliofanyika 16-6-2020 Jijini Dodoma
 RAIS wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania la 11, wakati wa hafla ya uvunjaji rasmin wa Bunge hilo, hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Bunge Jijini Dodoma 16-6-2020,( kulia kwa Rais) waliokaa Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano Mhe. Samia Sululu, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar. Mhe; Balozi Seif Ali Iddi na Spika wa Baraza la Wawakilishi. Mhe. Zuberi Ali Maulid
VIONGOZI  wa Wakuu wa Serikali kutoka Kushoto Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein,Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi, Spika wa Baraza la Wawakilishi.Mhe Zuberi Ali Maulid na Naibu Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Tulia Ackson, wakifuatilia hutuba ya Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Magufuli wakati wa hafla ya uvunjaji wa Bunge la 11.
WABUNGE wa Bunge la 11 wakifuatilia hutuba ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia kabla ya kulivunja Bunge hilo Jijini Dodoma
RAIS wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli akitoka katika ukumbi wa mkutano wa Bunge la 11, baada ya kumaliza hutuba yake ya kulivunja Bunge hilo akiongozana na Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein na Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, wakitoka katika ukumbi wa mkutano wa Bunge la 11 baada ya kuvunjwa rasman, wakiongozwa na Naibu Spika wa Bunge Mhe. Dk. Tulia Ackson



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.