Habari za Punde

Maandalizi ya sikukuu ya Eid el Hajj kisiwani Pemba

 BAADHI ya wananchi Kisiwani Pemba, wakinunua na wengine kuangalia nguo kwa ajili ya maandalizi ya skukuu ya Eid el Hajj katika maeneo ya mji wa Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 WANANCHI wakiwa katika moja ya mabanda ya kuuzia nguo kutoka kwa wafanyabishara wadogo wadogo wa soko la jumapili, mbele ya Hoteli ya Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 BIASHARA ya Mikungu, Vungu, na viotezo imekuwa kwa kasi katika kuelekea skukuu ya Eid el Hajj katika maeneo mbali mbali ya Chake Chake, pichani akinamama wakichagua bdhaa hizo.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 VIATU vya Kimasai vimekuwa vikipendwa na wananchi wengi, ikiwa ni moja ya utamaduni waviatu hivyo kuvaliwa na kanzu muda wa asubuhi wakati wa kwenda Msikitini kusali sala ya Eid, pichani mwananchi akiangalia viatu hivyo.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 IKIWA skukuu ya Eid el Hajj imefika, wananchi mbali mbali wakichagua viatu kwa ajili ya maandalizi ya skukuu hiyo, katika eneo la jua kali mjini Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 BIASHARA ya mayai imeonekana kuwa juu katika kipindi hiki cha kuelekea skukuu ya Eid el Hajj, ambapo treya mmoja inauzwa kati ya shilingi elfu 15,000/= hadi 14,000?=, pichani mmoja ya wauzaji wa mai hayo akimtilia mteja wake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

BIDHAA ya Samli,Siagi, Tomato Pest na viungo vya kupikia vyakula, vimekuwa ni kitu muhimu katika kuelekea skukuu pichani mmoja ya wafanya biashara akiwauzia wateja wake Tomato Pest kama alivyo kutwa katika eneo la mji ya Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.