Na
Mwandishi Wetu,
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Ranchi ya Taifa (NARCO), Masele Mipawa
amemsimamisha kazi Meneja wa Ranchi ya West Kilimanjaro iliyopo Arusha, Hezron
Kyaruzi kwa tuhuma za kukosa uadilifu kwa mali za Umma na kusababisha upotevu
wa Ng’ombe takriban 32.
Akiwa
katika ziara ya kutembelea Ranchi hiyo ya West Kilimanjaro mwishoni mwa wiki (Julai
18, 2020), Mipawa alisema kuwa waliamua kufanya maamuzi hayo kufuatia
changamoto nyingi zinazoikumba shamba hilo ambazo kwa kiasi kikubwa
zimechangiwa na uongozi mbovu wa meneja huyo.
“Kutokana
na upotevu wa Ng’ombe, uzembe na ukosefu wa maadili tumeamua kumsimamisha
kazi Meneja wa Ranchi na Msaidizi wake
na hatua nyingine za kisheria na
kinidhamu zitafuata,”alisema Mipawa
Mipawa
alisema ziara hiyo aliyoifanya katika Ranchi hiyo ni kufanya ukaguzi kutokana
na taarifa walizokuwa wakizipata ambazo zilionesha kuwa katika shamba hilo
kumetokea upotevu wa Ng’ombe ambao
Kampuni ya NARCO haina taarifa nao.
“Ziara
hii imetusaidia kubaini kuwa kuna wizi uliokithiri katika shamba hili ambao umechangiwa
na mahusiano mabovu kati ya Meneja na jamii inayozunguka shamba hili, ukosefu
wa maadili na uadilifu wa Meneja ambao umepelekea Ng’ombe 32 kupotea,”alisema
“Kati
ya ng’ombe hao 32 waliopotea 15 wameshapatikana na wengine 17 hawajapatikana
mpaka sasa huku ng’ombe wengine 27 walichinjwa bila kibali cha makao makuu,”alifafanua
Mipawa
Kufuatia
hali hiyo, Mipawa alisema wameamua pia kumsimamisha kazi Msaidizi wake kwa kuwa
alishindwa kumshauri vizuri meneja huyo huku ikidaiwa alikuwa akishirikiana na
meneja huyo kwenda kuazima ng’ombe kwa watu binafsi ili Ranchi hiyo ionekane ina
idadi kubwa ya ng’ombe.
Aidha,
Mipawa aliwataka wafanyakazi wengine waliobaki katika shamba hilo kuendelea
kufanya kazi kwa bidii, wazingatie nidhamu na uzalendo huku akiwaonya kuwa
Serikali ya Awamu ya Tano haitavumilia mtu yeyote anayehujumu rasilimali za
Taifa.
No comments:
Post a Comment