Habari za Punde

Umoja wa Vyama Vya Siasa Visivyo Rasmin Zanzibar Wazungumza na Waandishi wa Habari

Katibu wa Umoja wa Vyama vya Siasa visivyo rasmin Ameir Hassan Ameir amewataka wananchi kushirikiana na Rais wa awamu ya nane DK. Hussein Ali Mwinyi katika kuleta maendeleo ya Nchi  huko Ukumbi wa Wizara ya Habari Kikwajuni Zanzibar.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vyama vya Siasa visivyo rasmin Zanzibar Hussein Juma Salum ameipongeza Tume ya Uchaguzi Zanzibar kwa uchaguzi huru na kuridhishwa na matokeo ya Uchaguzi huo ,katika hafla ya mkutano na Waandishi wa Habari uliyofanyika Ukumbi wa Wizara ya Habari Zanzibar.

Katibu wa Umoja wa Vyama vya Siasa visivyo rasmin Zanzibar Ameir Hassan Ameir akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu matokeo ya Uchaguzi wa mwaka huu huko Ukumbi wa Wizara ya Habari Kikwajuni Zanzibar.

Na.Mwashungi Tahir    Maelezo         3-11-2020.

UMOJA wa vyama vya siasa  visivyo rasmin vimeipongeza Tume ya Uchaguzi wa Zanzibar kwa kufanya uchaguzi   huru  na wa haki   kuwafanya Wazanzibar kutumia Demokrasia yao ya kumchagua Dkt Hussein Ali Mwinyi   kuwa Rais wa Zanzibar.

Ameyasema hayo Katibu wa vyama vya siasa visivyo rasmin Ameir Hassan Ameir  wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari huko katika ukumbi wa Wizara ya Habari Utalii na Mambo ya Kale ulioko Kikwajuni.

Amesema kwamba Tume ya Uchaguzi Zanzibar  imeendesha uchaguzi huo kwa njia ya uhuru na amani  hadi kutangazwa Dr Hussein Ali Mwinyi  kuwa Rais wa awamu ya nane kwa kupata kura nyingi kwa asilimia 76 ambapo umoja huo umeridhika na maamuzi hayo.

Aidha Katibu huyo amesema uchaguzi umemalizika iliobakia wananchi kuendelea na pirika zao za maisha na kumpa mashirikiano kiongozi huyo aliyeingia madarakani.

“Uchaguzi umemalizika kilichobaki wazanzibar tushirikiane na kiongozi wetu huyu ili tuendeleze maisha yetu”, alisema katibu wa umoja huo.

Vile vile umoja huo umoja huo umewataka viongozi wote wa Chama cha Mapinduzi  walioteuliwa wakiwemo wakilishi, wabunge na madiwani kufanya kazi zao na kuwa na mashirikiano kwa wananchi wote ili tuijenge Nchi.

Hata hivyo umoja huo umefarijika na hotuba ya Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Ali  Mwinyi  aliyeitoa mara baada ya kuapishwa kwa kusema kuwa  atashirikiana na vyama vya siasa katika kuijenga Zanzibar.

Pia wamewataka wananchi wasipoteze muda wa kukaa vijiweni na kuwa na mategemeo ya kwamba uchaguzi utarejewa na kauli hiyo waifute kwani uchaguzi tayari umemalizika.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.