Habari za Punde

Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Wapatiwa Semina Elekezi Kufuatilia Miradi ya Maendeleo.

Na.Himid Choko. BLW 

Mkuu wa Kitivo cha Sheria  Chuo Kikuu cha Zanzibar Dkt Yahya Khamis Hamadi  amesema Wajumbe  wa Baraza la Wawakilishi wana wajibu wa kutambua na kufatilia kero na matatizo ya wananchi  na hatimae kuyapatia ufumbuzi kwa lengo la kuleta maendeleo katika majimbo  au makundi wanayoyawakilisha.

Akizungumza katika semina elekezi kwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi huko Chukwani , Dkt Yahya amesema miongoni mwa kazi za mwakilishi  ni kufuatilia miradi ya maendeleo iliyokubaliwa kutekelezwa katika maeneo yao.

Amesema katika wajibu kutimiza huo, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi hawana budi kutenga muda wao na kufanya vikao na wananchi wote wa maeneo yao ili kuwapa fursa wananchi kubadilishana mawazo na uwelewa pamoja na uzoefu kuhusiana na hali halisi zinazowakabili kwa lengo la kuyapatia ufumbuzi matatizo yako.

Amesema kwa kutumia rai hiyo, mjumbe anaweza kupata taarifa taarifa zitakazomuwezesha kujua vipaombele vya wananchi wa eneo lake na kufikisha taarifa hizo kwenye ngazi zinazohusika na utawala wa nchi kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi.

Amesema kwa misingi hiyo wajumbe wa Baraza la Wawakilishi lazima aweze kupambanua usahihi na umuhimu wa mambo yanayodaiwa na wananchi wa eneo lake.

Kuhusiana na Maadili ya Mwakilishi Dkt Yahya amefahamisha kwamba Mjumbe anatakiwa wakati wote kuzingatia maadili ya kazi zake ili pamoja na kulinda heshima ya Baraza na taifa kwa jumla kwa kuhakikisha kuwa hajiingizi katika vitendo vinavyoweza kulidhalilisha Baraza.

Amevitaja baadhi ya  vitendo hivyo ni pamoja na  rushwa, kashfa au matumizi ya lugha ya matusi, mavazi yasiyoheshimu mila, desturi na utamaduni wa Wazanzibari na mambo yanayofanana na hayo.

Mapema akitoa mada inayohusiana na Historian a Maendeleo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mkurugenzi wa Mashtaka ndugu Ibrahim Mzee Ibrahim amesema Maendeleo makubwa yamepatikana ikiwa ni pamoja na Kuongezeka kwa ushiriki wa wanawake hususan nafasi maalum kutoka 5  mwaka 1980 hadi  kufikia asilimia 40% (nafasi 20 ) hivi sasa na kuongezeka kwa idadi ya wajumbe wawakilishi waliochaguliwa na wananchi moja kwa moja kutoka wajumbe 10 mwaka 1980 ililipoanzishwa baraza hilo hadi kufikia 50 hivi sasa.

Mafunzo hayo yataendeleo hapo kesho.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.