Habari za Punde

Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Kutoka Chama cha ACT-Wazalendo Wafanya Usajili Ofisi za Baraza Chukwani leo.

Afisa wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar akiwafanyia Usajili Wajumbe Wateule wa Baraza la Wawakilishi Zanzibat kutoka Chama cha ACT-Wazalendo Jimbo la Kojani Mhe. Hassan Hamad Omar na Mwakilishi Mteule wa Jimbo la Wingwi Mhe.Kombo Mwinyi Shehe na Mwakilushe Mteule wa Jimbo la Mtambile Mhe. Habibu Ali Mohammed, walipofika katika Ofisi za Baraza kwa ajili ya kufanya usajili na kuriupoti  leo kwa hatua nyengine za uapishaji.

Katibu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar ndugu Raya Issa Msellem akizungumza na Wawakilishi wateule kutoka chama cha ACT wazalendo Jimbo la Kojani Mhe.Hassan Hamad Omar,  Jimbo la Mtambile Mhe. Habibu Ali Muhamed na Jimbo la Wingwi Mhe.  Kombo Mwinyi Shehe mara baada ya kusajiliwa.


Msimamizi wa Maktaba ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar ndugu Haji Khatibu Haji akiwafahamisha Wawakilishi wateule kutoka chama cha ACT wazalendo jinsi wanavyoweza kupata huduma katika maktaba hiyo kwa ajili ya shughuli zao.

Afisa uhusiano wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar ndugu Himidi Choko akiwapa maelezo Wawakilishi wateule kutoka chama cha ACT wazalendo kuhusu mambo mbali mbali yanayowahusu ukaaji wa wajumbe ndani ya ukumbi  wa Baraza la Wawakilishi Chukwani.

                                                                 Picha na Masoud Hamad -BLW -Zanzibar.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.