Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi Ajumuika na Wananchi wa Kijiji cha Bweleo Katika Sala ya Ijumaa leo 5-2-2021.

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Wazee wa Kijiji cha Bweleo alipowasili katika viwanja vya Msikiti Mkuu wa Ijumaa Bweleo kwa ajili ya Ibada ya Sala ya Ijumaa iliofanyika katika Kijiji cha Bweleo leo 5-2-2021.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwasalimia na kuzungumza na Wananchi wa Kijiji cha Bweleo Wilaya ya Magharibi “B” Unguja baada ya kumalizika kwa  Sala ya Ijumaa iliofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Bweleo.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi na Waumini wa Kiislam wakifuatilia mawaidha yakitolewa na Katibu wa Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khalib Ali Mfaume, baada ya kumalizika kwa Sala ya Ijumaa iliofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Bweleo Wilaya ya Magharibi “B” Unguja.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi akiitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi (kulia kwa Rais) baada ya kumalizika kwa Sala ya Ijumaa iliofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Bweleo Wilaya ya Magharibi “B” Unguja na (kushoto kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Idrisa Mustafa Kitwana.
WAUMININ wa Kiislam wakiitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh. Saleh Omar Kabi (hayupo pichani) baada ya kumalizika kwa Sala ya Ijumaa iliofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Bweleo Wilaya ya Magharibi “B” Unguja.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi akiondoka katika viwanja vya Msikiti Mkuu wa Ijumaa Bweleo baada ya kumaliza Sala ya Ijumaa iliofanyika katika msikiti huo leo 5-2-2021, na kujumuika na Wananchi wa Kijiji hicho.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.