RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Wazee wa Kijiji cha
Bweleo alipowasili katika viwanja vya Msikiti Mkuu wa Ijumaa Bweleo kwa ajili
ya Ibada ya Sala ya Ijumaa iliofanyika katika Kijiji cha Bweleo leo 5-2-2021.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwasalimia na kuzungumza na Wananchi wa
Kijiji cha Bweleo Wilaya ya Magharibi “B” Unguja baada ya kumalizika kwa Sala ya Ijumaa iliofanyika katika Msikiti Mkuu
wa Ijumaa Bweleo.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi na Waumini wa Kiislam wakifuatilia
mawaidha yakitolewa na Katibu wa Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khalib Ali
Mfaume, baada ya kumalizika kwa Sala ya Ijumaa iliofanyika katika Msikiti Mkuu
wa Ijumaa Bweleo Wilaya ya Magharibi “B” Unguja.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi akiitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa
Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi (kulia kwa Rais) baada ya kumalizika kwa Sala
ya Ijumaa iliofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Bweleo Wilaya ya Magharibi
“B” Unguja na (kushoto kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe.
Idrisa Mustafa Kitwana.
WAUMININ wa Kiislam wakiitikia dua ikisomwa na
Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh. Saleh Omar Kabi (hayupo pichani) baada ya
kumalizika kwa Sala ya Ijumaa iliofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Bweleo
Wilaya ya Magharibi “B” Unguja. RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi akiondoka katika viwanja vya Msikiti
Mkuu wa Ijumaa Bweleo baada ya kumaliza Sala ya Ijumaa iliofanyika katika
msikiti huo leo 5-2-2021, na kujumuika na Wananchi wa Kijiji hicho.
No comments:
Post a Comment