Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi Ametembelea Nyumba za Maafa Tumbe Wilaya ya Micheweni Pemba leo.

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akitembelea moja ya Nyumba za Maafa Tumbe akipata maelezo ya Mradi huo kutoka kwa Katika Mkuu Ofisi  ya Makamu wa Pili wa Rais Sera Uratibu na Baraza la Wawakilishi Ndg. Thabit Idarous Faina, alipofanya ziara kutembelea Mradi huo

Pemba                                                          12.03.2021

---

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi, amewataka wananchi watakaokabidhiwa nyumba za vijiji za maafa zilizojengwa Tumbe Kisiwani Pemba na Nungwi kwa Unguja, kuhakikisha nyumba hizo wanazitunza ili zisipoteze haiba yake.

 

Rais Dk. Mwinyi alisema nyumba hizo hivi karibuni zinatarajiwa kuzinduliwa kwa upande wa Unguja ikiwa ni pamoja na Pemba, ili wananchi waliokusudiwa waweza kuzitumia.

 

Aliyaeleza hayo leo mara baada ya kumaliza ziara ya kukagua nyumba hizo 15 ambazo zitakaliwa na familia 30, zilizoko katika kijiji cha Tumbe Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, wakati waziara yake ya siku moja Kisiwani Pemba.

 

Aidha, Rais Mwinyi aliwashukuru wananchi wa Shehia ya Tumbe kuonyesha kuwa wapo tayari kwa ushirikiano na Serikali yao, huku akisema kwamba changamoto zilizopo katika nyumba hizo zinashuhulikiwa ili kumailizika kwa wakati.

 

“Tumeambiwa kama suala la maji ni changamoto kwa sasa, ila hivi karibuni litamalizika, fedha za fidia nazo zinashuhulikiwa ndani ya wiki hii zinamalishwa na changamoto ya idadi ndogo ya watu wanaohitaji kuwepo hapa nayo inashuhulikiwa”alisema.

 

Katika hatua nyengien Dk.Mwinyi aliwashukuru wafadhili waliojenga nyumba hizo, Emirates Red Creasent ya Falme za Kiarabu kwa kazi kubwa walioifanya, kuhakikisha nyumba hizo wameziwekea na huduma za kijamii ikiwemo, kituo cha afya cha kisasa, skuli, msikiti na maduka.

Akizungumzia suala la Amani na Utulivu, Dk. Mwinyi aliwataka wananchi wa Unguja na Pemba, kuendelea kudumisha amani iliyopo, Umoja na mshikamano, kwani lengo la serikali ya Umoja wa Kitaifa ni kuwaunganisha watu, kwa kuachana na mifarakano iliokuweopo.

 

“Tumefanya hivi ili kuwaweka wananchi katika hali ya amani, utulivu na usalama ili waweze kupata maendeleo yaliokuwa bora kutka kwa viongozi wao”alisema.

 

Hata hivyo, Rais Dk. Mwinyi alisema kuwa hatua iliyobaki hivi sasa ni serikali kupeleka maendeleo kutokana na kuwepo kwa amani, umoja na mshikamano, huku akitambua kuwa kuna huduma nyingi za kijamii zinazohitajika, ikiwemo afya, maji, elimu barabara na hususan za vijijini, kwani aliwaahidi wananchi wakati wakampeni kwamba atahakikisha kuwa huduma hizo zinapatikana.

 

Kwa upande wa akinamama aliwahidi kuwa Serikali itawapatia mikopo kutoka mabenki, hivyo wanapaswa kujipanga vyema katika vikundi vyao, kwa kuwapatia mafunzo, mitaji na masoko, kitu watakachopewa kitakuwa na tija nao.

 

Nae Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Sera Uratibu na Baraza la Wawakilishi Dk. Khalid Salum Mohamed, alisema kuwa nyumba hizo 15 zinazochukua familia 30 kwa wakati mmoja, pia kuna hospitali ya kisasa, soko, maduka 15, msikiti unaochukua watu 350 pamoja na skuli yenye vyumba tisa.

 

Dk. Khalid alisema chanzo cha ujenzi wa nyumba hizo ni athari zilizotokea mwaka 2017 za mvua kubwa ya masika, ambayo karibu familia 6500 unguja na Pemba ziliathiria, lakini watu wa Mwezi Mwekundu walikuja na kushirikiana na serikali kujenga nyumba za kuwasaidia waathirika hao.

 

Alieleza kuwa waathirika ni wengi lakini ilionekana familia 385 ambao nyumba zao ingebidi vivynje kutokana kuwepo katika maeneo hatarishi, Pemba nzima imeoneka kuna familia 41 nyumba hizo na hao wapate makaazi hapa.

 

Aidha, alisema kuwa mradi kama huo upo huko Nungwi kwa upande wa Unguja, na kueleza kuwa kwa mujibu wa mkataba serikali imelazimika kutengeneza barabara, Kupeleka umeme na maji ambapo kwa upande wa maji tayari visima vitatu wameshachimbwa ila hawakufanikiwa kutokana na uhaba wa maji, lakini hivi sasa wanachimba chengine na kwenda hadi mita 90 na wanatarajia kuyakuta maji.

 

Kwa upande wa fidia, Waziri huyo alisema tayari wameshalipa TZS Milioni 16 na TZS Milioni 11 wanatarajia kuzimaliza ndani ya wiki inayofuata, kati ya milioni 27 walizokua wakidaiwa kwa ajili ya fidia.

 

Wakati huo huo, Rais Dk. Mwinyi alifika Mtaa wa Mpendae Mjini Unguja kwenda kutoa mkono wa pole kwa familia ya Marehemu Dk. Idrissa Ahmada Khamis aliyefariki dunia hapo jana na kuzikwa leo huko kijijini kwao Kinduni Mkoa wa Kaskazini Unguja.

 

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 

 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.