Habari za Punde

Serikali ya Ujerumani Kutoa Bilioni 56 Kusaidia Uhifadhi Nchini.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro ( wa kwanza  kulia)  akiwa na Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Mhe.Regine Hess ( wa pili kushoto)  wakimsikiliza ....Mratibu wa wa Frankfurt Zoological Society Jack Ryan wakati  akitoa maelezo katika Viongozi wakati walipotembea Karakana iliyopo katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti inayoendeshwa na Shirika la Kimataifa la Uhifadhi la Frunkfurt Zoological Society iliyofadhiliwa na Serikali ya Ujerumani
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro akizungumza na Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Regine Hess wakati wakitembelea miradi mbalimbali iliyopo ndani na nje ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti  inayofadhiliwa na Serikali ya Ujerumani 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro akiwa na  Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Mhe.Regine Hess wakimsikiliza Kamishna Mwandamizi wa Uhifadhi wa Kanda Maghraibi, Martin Looiboko wakati wakitembelea miradi mbalimbali iliyopo ndani na nje ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti  inayofadhiliwa na Serikali ya Ujerumani 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro akiwa kwenye picha ya pamoja na  Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Regina Hess  mara baada yaembelea miradi mbalimbali iliyopo ndani na nje ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti  inayofadhiliwa na Serikali ya Ujerumani 

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt.Allan Kijazi akimsikiliz  Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Regine Hess  kabla ya kuanza  kutembelea miradi mbalimbali iliyopo ndani na nje ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti  inayofadhiliwa na Serikali ya Ujerumani 

Na.lusungu helela   

Serikali ya Ujerumani inatarajia kutoa  kiasi cha Yuro Milioni 20 sawa na  Shilingi  Bilioni 56 za Kitanzania  zitakazotumika kwa ajili ya miradi ya mikubwa ya  shughuli za Uhifadhi nchini.

Akizungumza leo na Waandishi wa Habari katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti liliyopo wilaya ya Serengeti mkoani Mara Waziri wa Maliasili na utalii,,Dkt.Damas Ndumbaro akiwa na Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania amesema miradi  mbalimbalii inayofadhiliwa na Ujerumani iliyopo ndani na nje ya Hifadhi ina umuhimu mkubwa katika Uhifadhi

Amesema fedha hizo zitatumika kwa ajili ya kuangalia mradi wa Ikolojia ya   Serengeti  pamoja na mradi wa Ikolojia ya Mwl.Nyerere ( Selous) 

Dkt. Ndumbaro amesema msaada huo ni muendelezo wa ushirikiano baina ya Tanzania na Ujerumani   katika masuala ya Uhifadhi uliodumu kwa zaidi ya miaka 60

Amesema msaada huo wa fedha h utalinufaisha Shirika la Hifadhi za Taifa ( TANAPA) Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania ( TAWA) pamoja na Shirika la Kimataifa la Uhifadhi la  Frankfurt Zoological Society ( FZS) 

Aidha, Waziri Dkt.Ndumbaro amesema mbali ya fedha hizo kutumika katika masuala ya Uhifadhi, Serikali ya Ujerumani imejipanga pia kuzinufaisha Jamii zinazoishi kuzunguka Hifadhi.

Amesema nchi ya Ujerumani ni miongoni mwa Wadau wakubwa wa Uhifadhi nchini ambao wamekuwa wakisaidia masuala mengi  katika Uhifadhi ikiwemo tafiti mbalimbali pamoja na vita dhidi ya Ujangili

" Tunaishukuru sana Serikali ya Ujerumani kwa msaada wao kama Wizara na Serikali ya Tanzania kwa ujumla tunasema asante sana " alisema Dkt.Ndumbaro

Amefafanua kuwa mradi huo utadumu kwa muda wa miaka mitatu na unatarajia kuanza hivi mapema mara baada ya bajeti kupitishwa.

katika hatua nyingine, Waziri Dkt.Ndumbaro amesema katika Azimio la Arusha Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kusemam  kuwa shughuli za Uhifadhi zinahitaji ushirikiano wa Wadau kwa ajili ya kutoa fedha pamoja na utalaamu.

Kwa upande wake, Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Mhe. Regine Hess amesema msaada huo utasaidia Hifadhi hizo katika kipindi  hiki cha mlipuko waa Ugonjwa wa Kovid ambapo idadi ya  watalii imepungua.

Ameongeza kuwa Serikali ya Ujerumani  imetoa fedha hizo kwa ajili ya  kusaidia  Hifadhi hizo ikiwa ni kuenzi misingi ya ushirikiano iliyowekwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere  

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.