Habari za Punde

BUNGE LAPITISHA BAJETI KUU YA SERIKALI KWA MWAKA 2021/22

Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akijibu hoja wakati wa kuhitimisha mjadala wa Bajeti Kuu ya Serikali ya Sh. trilioni 36.66 kabla ya Bunge kuidhinisha Bajeti hiyo Bungeni jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Naibu wake, Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (Mb) wakiteta jambo kabla ya wabunge kuipitisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka 2021/22, bungeni jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (Mb) akijibu hoja kabla ya kupitishwa kwa Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka 2021/22 ya shilingi trilioni 36.66, bungeni jijini Dodoma.
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa (Mb) akimpongeza Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) baada ya kuhitimisha kujibu hoja za wabunge kuhusu mapendekezo ya Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2021/22, jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akipewa zawadi na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Dorothy Gwajima (Mb), Bungeni jijini Dodoma baada ya kujibu hoja za wabunge kuhusu kodi zilizopendekezwa katika Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2021/22.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (kulia), akiteta jambo na viongozi wa Wizara hiyo, wa pili kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Emmanuel Tutuba na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Adolf Ndunguru, baada ya Bunge kupitisha Bajeti Kuu ya Serikali ya Sh. trilioni 36.66, kwa mwaka 2021/22, bungeni jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akipongezwa na Mama Salma Kikwete (Mb) baada ya Bunge kupitisha Bajeti Kuu ya Serikali ya Sh. trilioni 36.66, kwa mwaka 2021/22, bungeni jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Adolf Ndunguru (katikati) akiteta jambo na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Khatib Kazungu (kulia), wa pili kushoto ni Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, Bw. Alphayo Kidata na Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Mipango wa Wizara hiyo Bw. Moses Dulle, jijini Dodoma.

Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Naibu wake Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (Mb), wakiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara na Taasisi za Wizara ya Fedha na Mipango, baada ya Bunge kupitisha Bajeti Kuu ya Serikali ya Sh. trilioni 36.66, kwa mwaka 2021/22, bungeni jijini Dodoma.

(Picha na Peter Haule, WFM, Dodoma) 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.