Baadhi ya Waandishi wa habari wakiskiliza Ufafanuzi uliyotolewa na Naibu Katibu Mkuu kutoka Chama cha Walimu Zanzibar (ZATU) Salim Ali Salim (hayupo pichani) juu ya tukio lilotokea katika Skuli ya Sunni Madrasa iliyopo Mkunazi Mkoa wa Mjini Magharibi hafla iliyofanyika katika Ofisini za Chama hicho Kijagwani Zanzibar.
Na Kijakazi Abdalla Maelezo
Chama cha Walimu Zanzibar (ZATU),wameziomba mamlaka zinazosimamia makosa ya kinidhamu kutumia busara wakati wakishughulikia mashauri ya kada ya ualimu.
Akizungumza na Waandishi wa Habari katika ofisi za chama hicho, huko Kijangwani Mjini Unguja, Naibu Katibu Mkuu wa ZATU, Bwana Salim Ali Salim kufuatia tukio la kupigwa kwa Mwalimu wa Skuli ya Sunni Madrasa na mzee wa mwanafunzi anayesoma katika Skuli hiyo.
Amesema kua walimu ni washirika wakubwa wa kuhakikisha watoto wanapata elimu iliyo bora ili kuona taifa linapata wasomi wazuri.
Amesema kufuatia kwa kupigwa kwa Mwalimu Chama cha Walimu Zanzibar, kimeiomba Wizara ya Elimu Zanzibar inaposhughulikia migogoro ya walimu busara zitumikie ili kuepusha uhasama na kuharibu ufanisi wa kada ya uwalimu.
Alieleza kuwa, Chama hicho kinasikitishwa kwa baadhi ya wazazi kuingia katika maeneo ya skuli na kuwashambulia walimu kwa kisingizio kuwa watoto wamepigwa
No comments:
Post a Comment