Habari za Punde

Mzee Sadalla Juma Sadalla (74) Aliyembaka mfanyakazi wake wa nyumbani Unguja, arudishwa rumande

 Mshitakiwa Bwana Sadalla Juma Sadalla mwenye umri wa miaka 74 aliyembaka mfanyakazi wake wa nyumbani (house Girl) mwenye umri wa miaka 15

Alifikishwa mahakamani tena leo 31 Augosti 2021 katika mahakama ya Vuga,Unguja. na baada ya kusimamishwa kizimbani Hakimu ameamru mshitakiwa arudishwe mahabusu hadi tarehe 19 Septemba 2021 kesi hiyo itakaposikilizwa tena.

Mshitakiwa Bwana Sadalla Juma Sadalla anashitakiwa kwa kumbaka msichana wake wa kazi (jina linahifadhiwa).

Bwana Sadalla Juma Sadalla ameripotiwa  na analalamikiwa na kuwa ni mzoefu wa tabia za ubakaji na mara nyingi kesi zake huzimaliza kienyeji lakini mara hii vyombo vya dola katika kukomesha vitendo vya ubakaji vimemtia nguvuni na kumfikisha  mbele ya vyombo vya sheria.

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeazimia kukomesha kabisa vitendo vya ubakaji,udhalilishaji wa kijinsia.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.