Habari za Punde

Serikali kufanya uhakiki wa vikundi vilivyoomba Mikopo ya Uviko 19

 

TAARIFA YA MHESHIMIWA WAANDISHI WA HABARI WA KUHUSU ZOEZI LA UHAKIKI WA VIKUNDI VILIVYOOMBA MIKOPO YA UVIKO 19 AMBALO LITAFANYIKA  KUPITIA MIKOA MITATU YA UNGUJA KUANZIA TAREHE 06/12/2021

 

Ndugu Waandishi wa Habari,

Ndugu Wananchi,

Mabibi na Mabwana,

Assalaamu Alaykum.

Awali ya yote sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia neema ya uzima na  Afya njema na kukutana hapa asubuhi. Naomba nikushukuruni nyote kwa kuitikia wito wetu wa kuungana nasi ili kupokea taarifa zetu mbalimbali za Afisi yetu.

Ndugu Waandishi wa Habari;

Lengo la kukutana nanyi hapa ni kukupeni taarifa kuhusiana na zoezi linalotakiwa kufanywa na Afisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji kwa kushirikiana na Afisi za Mikoa na wadau wengine wanaohusiana na Programu ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi la kufanya Uhakiki wa Vikundi vilivyoorodheshwa juu ya uhitaji wa kupatiwa mikopo ya fedha zilizotokana fedha za Mkopo wa IMF za ahueni ya janga la Uviko 19 ambapo Serikali yetu imezipokea na kuzisimamia.

Kama mnavyofahamu fedha hizi zimelengwa kuwanufaisha wananchi wote wa Zanzibar (Unguja na Pemba) ambao wanaohitahi wa fedha hizo na wamekidhi vigezo vilivyowekwa. Aidha fedha hizo ni za masharti mepesi ili wananchi wenye uwezo mdogo/duni kufaidika.

Ndugu Waandishi wa Habari;

Napenda kueleza kuwa wananchi wengi kupitia vikundi vyao wameshajihika na kuomba kupatiwa fedha hizo. Nachukua fursa hii kuzishukuru Asasi mbalimbali za Umma na Binafsi kuwashajihisha Wananchi. Shukrani za pekee napenda kuzitoa kwa Serikali za Mikoa na Wilaya kwa kazi kubwa walioifanya kuhusu jambo hili la kuwashajihisha wananchi. Pia nina  kushukuruni sana Nyinyi waandishi kwa ufanisi mkubwa wa kuwaeleza wananchi juu ya fedha za COVID 19 au UVIKO 19.

Ndugu Waandishi wa Habari;

Kwa kuwa fedha hizi za UVIKO 19 ni za Serikali hivyo watapatiwa wananchi kupitia vikundi vyao, kabla ya fedha hizo kutolewa Afisi yangu, Afisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji kwa kushirikiana na  Serikali za Mikoa na Wadau wengine kuanzia Jumatatu tarehe 06 Disemba,2021 tutafanya zoezi la Uhakiki kwa vikundi vyote viliomba na kuorodheshwa kupata mikopo.

Ndugu Waandishi wa Habari;

Uhakiki huu itaangalia na kupitia taratibu na miongozo iliowekwa  Serikali kupitia Afisi ya Rais,Kazi,Uchumi na Uwekezaji kwa kushirikiana na Wizara zinazohusika moja kwa moja na sekta zilizomo katika mradi huu.Vigezo hivyo uwepo wa kikundi au ushirika ulio rasmi wenye kutambulika kisheria kwa kupata usajili ,uwepo wa Biashara ,kikundi kiwe na uhitaji wa mkopo huo pamoja na kufuata taratibu za maombi ili kuweka misingi imara ya uwezeshaji Wananchi kiuchumi.

Ndugu Wananchi na Ndugu Waandishi wa Habari;

Napenda kukujulisheni ili nanyi muweze kuwaeleza Wananchi wetu kwamba, kwa wote waliomba kupatiwa fursa ya fedha hizi za UVIKO 19 wanapaswa kutambua kwamba mikopo hii ni yenye masharti nafuu ili kuweza kuimarisha uzalishaji wa bidhaa na utoaji wa huduma kwa lengo la kujiajiri na kuzalisha ajira,hivyo Serikali za Mikoa tayari zimetoa mashirikiano kwa kuwataarisha wajasiriamali wetu kupitia shehia mbali mbali ili kuweza kunufaika na fedha hizi.

Ndugu Waandishi wa Habari;

Mbali na kuwekwa kwa taratibu hizo, Afisi ya Rais,kazi,Uchumi na Uwekezaji kwa kushirikiana na Wadau pamoja na Serikali za Mikoa, imeanza utaratibu wa awali wa kuhakiki vikundi vyote ambavyo vimewasilishwa kutoka mikoani kupitia shehia mbali mbali ili kuhakikiwa na wajumbe kutoka Kamati ya Ufuatiliaji ili kujiridhisha juu ya uwepo wa vikundi na shughuli zake,baadae kufanyiwa tathmini itakayofanywa na Watendaji wa Benki, Mfuko na Watendaji wengine watakaoteuliwa katika kazi hiyo. Ili kujua kiasi gani cha fedha kinahutajika kwa mradi ulioomba.

Ndugu Wananchi na Ndugu Waandishi wa Habari;

Napenda kuwajuulisha wananchi ambao wamejitokeza katika kuorodhesha vikundi vyao kupitia Serikali za Mikoa kwamba zoezi la uhakiki wa vikundi litafanyika kuanzia siku ya jumatatu  na tarehe 06/12/2021 kwa Mkoa wa Kusini Unguja na kufuatiwa na mikoa mengine ya Kaskazini na Mjini Magharibi.Aidha napenda kuwaomba wajasiriamali wetu kutoa mashirikiano ili kuhakikisha zoezi hilo linafanyika kwa lengo la kukamilisha program hii na kuhakikisha vikundi vya wajasiriamali mbali mbali walioainishwa wananufaika kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa zoezi la kuhakiki ni endelevu kwa sababu program za Uwezeshaji nazo ni endelevu.Kwa hivyo  naomba viongozi tuwaelimishe na kuwatayarisha wajasiriamali wetu ili waweze kushiriki kikamilifu katika program hii.

Ndugu Wananchi na Ndugu Waandishi wa Habari;

Zoezi hili ni la kawaida kama Utafiti na Ufuatiliaji mwengine unavyofanywa hivyo wananchi wasiwe na wasiwasi wawote. Natoa wito kwa kushiriki zoezi hili na kutoa taarifa sahihi kwa manufaa yao, Serikali na Wananchi wote. Serikali ipo kwa ajili yao, itawalinda, kuwaenzi na kuwasaidiwa kadri hali inavyoruhusu.

Ahsanteni sana kwa kunisikiliza na kuwaombeni ushirikiano wenu mkubwa.

 

 

AHSANTENI SANA KWA KUNISIKILIZA


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.