Habari za Punde

TASAC YAWATAKA WAFANYABIASHARA MPAKANI KUACHA KUTUMIA NJIA ZA PEMBENI KUPITISHA MIFUGO

MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala wa Shirika la Meli Tanzania (TASAC) Captain Mussa Mandia kulia akisisitiza jambo wakati wa ziara yake mpakani mwa Tanzania na Kenya eneo la Horohoro
MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala wa Shirika la Meli Tanzania (TASAC) Captain Mussa Mandia kulia akipata maelezo kutoka kwa Afisa Mfawidhi wa TASAC Mkoa wa Tanga Captain Christopher Shalua wakati wa ziara yake mpakani mwa Tanzania na Kenya eneo la Horohoro
MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala wa Shirika la Meli Tanzania (TASAC) Captain Mussa Mandia kushoto akimsikiliza kwa umakini mmoja wa watumishi wanaofanya kazi eneo la mpakani kupitia wakala huo wakati wa ziara yake mpakani mwa Tanzania na Kenya eneo la Horohoro

NA OSCAR ASSENGA, MKINGA

MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala wa Shirika la Meli Tanzania (TASAC) Captain Mussa Mandia amewataka wafanyabiashara wa mifugo mipakani nchini kutoa ushirikiano kwa wakala huo huku ikiwataka pia kuacha tabia ya kutumia njia za pembeni badala yake wapitishe kwenye mpaka huo ili serikali iweze kupata mapato yake

Captain Mandia aliyasema hayo leo wakati wa ziara yake kutembelea mpaka huo unaotenganisha kati ya nchi ya Tanzania na Kenya eneo la Horohoro ili kuweza kujifunza na kuona shughuli zinazofanyika kwenye maeneo ya mpaka huo.

Akiwa kwenye mpaka huo aliwatataka wafanyabiashara waongeza ushirikiano ili kuiwezesha Serikali iweze kukusanya mapato yake ikiwemo kuacha kutumia njia pembeni kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria

“Kama leo nipo hapa mpakani wa Kenya na Tanzania eneo Horohoro nimeambiwa usafirishaji mifugo umepungua sana kutoka 10,000 mpaka 3000 sawa na asilimia 30 ya mifugo sababu kubwa ni ukwepaji wa kupitisha mifugo kwenye kituo hiki kwa sababu mbalimbali

Mwenyekiti huyo wa bodi alisema wao kama Wakala wataliangalia hilo na kujaribu kuboresha mazingira na kuhakikisha wafanyabiashara wanafaidika na serikali haipotezi mapato.

“Niwaambie kwamba acheni kutumia njia za pembeni mkiwa na malalamiko yenu yafikisheni kwetu nasi tutaona namna bora ya kuboresha biashara ya mifugo hapa mpakani “Alisema Mwenyekiti huyo wa Bodi.

Aidha alionyeshwa kufurahishwa na hatua ya wakala huo mpakani hapo kushirikiana vema na mamlaka nyengine zilizopo mpakani na kuweza kuboresha makusanyo ya kodi ya nchi yetu yameonekana kwa asilimia 500 ndani ya mwaka mmoja.

Alisema hilo ni jambo muhimu na linahitaji kutazamwa kwa jicho zuri zaidi ili kuweza kuliendeleza na kuongeza wigo mkubwa zaidi ya ukusanyaji wa mapato ya serikali.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.