Habari za Punde

ZANTEL yahimiza wafanyabiashara kutumia huduma ya Lipa kwa Simu ili kuongeza mapato.

 

Mtaalamu wa huduma ya Ezypesa Zantel  Eunice Hubert Alelyo akiwaelekeza wafanyabiashara jinsi ya kujisajili na huduma ya Lipa kwa Simu katika mkutano uliofanyika Kiembesamaki,Unguja.
Baadhi ya mawaka waliokwisha kujisajili na huduma ya Lipa kwa simu wakiwa katika picha ya Pamoja. 

Mmoja wa wafanyabiashara Rabia Burhan akielezea faida alizozipata tangu ajiunge na huduma ya Lipa kwa Simu,akibainisha ni kwa namna gani huduma ya Lipa kwa simu imemsaidia kuongeza wateja na mapato katika biashara yake.

KAMPUNI ya simu za mkononi Zantel kupitia huduma ya lipa kwa simu imesema inathamini mchango wa wafanyabiashara wanaotumia huduma hiyo na kurahisisha mchakato mzima wa utoaji huduma kwa wateja.                                                                                                                                                          

Kauli hiyo ilitolewa na Mtaalamu wa Huduma ya Ezypesa wa Zantel Eunice Hubert Alelyo, wakati akizungumza katika mkutano wa wafanyabiashara mbalimbali wanaotumia huduma ya lipa kwa simu huko Kiembesamaki,Unguja.

Alisema huduma hiyo ina faida kubwa hasa uhifadhi na usalama wa fedha za mfanyabiashara hivyo ni vyema kuitumia ili kukuza soko la fedha na kumrahisishia mteja kuitumia muda wowote anapohitaji bidhaa.

Aidha alisema lengo kubwa la mkutano huo ni kutoa elimu kwa wafanyabiashara wanaotumia huduma ya lipa kwa simu ambao bado hawana uelewa wa kina juu ya umuhimu na faida za huduma hiyo .

Eunice alibainisha kwamba huduma hiyo inawahusu zaidi wafanyabiashara wa Zanzibar wanaotoa huduma mbalimbali za kibiashara ikiwemo nguo, mikahawa na inamsaidia mfanyabiashara kukusanya mapato yake kwa urahisi.

Alisema hadi sasa wana wafanyabiashara zaidi ya 4000 hasa katika maeneo ya mjini ambao wameipokea huduma hiyo lakini pia kwa upande wa Pemba katika maeneo ya Wete na Chake Chake pia wameipokea kwa muamko mkubwa.

Kwa upande wake, Yassir Baharudin, mtaalamu wa teknolojia ya mtandao, alisema kuwa kutokana na kukua kwa huduma za intaneti, ni muhimu kwa wafanyabiashara kujiunga na huduma hii adhimu ili kurahisisha mchakato mzima wa kufanya biashara.

‘’Huduma hii ni salama na inarahisisha kazi sana ukilinganisha na malipo ya kawaida, inaokoa muda na usumbufu wa kurekodi kila manunuzi anayofanya mteja. Kutokana na kukua kwa teknolojia jambo hili limewezekana na ni muhimu kwenu nyinyi wafanyabiashara kulipokea na kuhakikisha mmejisajii katika huduma hii ya Lipa kwa simu na Zantel.”

Nao wafanyabiashara wanaotoa huduma zao kupitia mtandao walisema huduma hiyo kwa kiasi kikubwa inarahisisha utoaji wa huduma kwa wateja wao.

Rabia Burhan Saleh alisema awali alikuwa akipata changamoto kubwa katika biashara yake lakini hivi sasa anafurahishwa na huduma hiyo kwani ina faida kubwa hivyo anatoa wito kwa wafanyabiashara wengine kujiiunga na huduma hii kwani ina faida kubwa kwao na haina makato.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.