Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi Ahudhuria Maadhimisho ya Miaka 25 ya Taasisi ya Mfuko Fursa Sawa kwa Wote.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Mwenyekiti wa Taasisi ya Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote  (EOTF) Mama Anna Mkapa, baada ya kuwasili katika viwanja vya Ukumbi wa Mikutano wa  Kimataifa wa Mwalimu Julias Nyerere Jijini Dar es Salaam kuhudhuria hafla ya Maadhimisho ya miaka 25 tangu kuanzishwa kwa Mfuko huo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akielekea katika sehemu ilioandaliwa kwa hafla ya Maadhimisho ya Miaka 25 ya Taasisi ya Mfuki wa Fursa Swa kwa Wote (kushoto kwa Rais) Mwenyekiti wa Taasisi ya Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote  (EOTF) Mama Anna Mkapa na (kulia kwa Rais) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akitembelea Maonesho ya Bidhaa za Wajasiriamali  mbalimbali wakati wa hafla ya Maadhimisho ya Miaka 25 ya Taasisi ya Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote, yaliofanyika katika ukumbi wa  Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.




 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.