Habari za Punde

Toa Sadaka yako kukamilisha ujenzi wa Madrssa Hii Kengeja Pemba

 

Muonekano wa Majengo ya Madrasa Katika Kijiji cha Kengeja Kisiwani Pemba yakisubiri mchango wako ili kuweza kukamilika kwa ujenzin huo na kuaza kutowa Elimu ya Dini kwa Wananchi na Watoto wa Kijiji hicho. Sadaka yako ni muhimu katika ujenzi huo na kutoka Sadaka yako ili kuweza kujiwekea kwa Mola. 

Enzi za uhai wake Marehem Baba yetu  alitoa eneo hili lililojengwa Madrassa ambayo imekamilika na kuendelea kusomewa  masomo ya Dini ya Kiislam hivi sasa,eneo jengine linaloendelea kujengwa madrassa vile vile ni sehemu tulioendeleza kutoa sisi warithi kama sadaka yetu  tena.

Ujenzi wa eneo hili hauna mfadhili isipokua wenye kuitengenza Akhera yao hujitoa na kusahau ya Dunia na kuwekeza zaidi kwa Mwenyezimungu.

Nikuombe wewe unaesoma ujumbe huu kutoka ulichonacho ili kuwa sehemu ya waliotoa sadaka zao kukamilisha majengo haya ambayo matumizi makubwa yatakua ni kusomewa dini ya kiislamu na wanafunzi kutoka maeneo mbali mbali ya Pemba na nje ya Zanzibar kuishi hapa ambao hivi sasa wamekodiwa nyumba kama hostel yao.

Madrssa hii ya Fatuma Bint Rasuul ipo kijijini kengeja kitongoji cha mwakunguu na inahitaji mabati ya kawaida,milango saruji na mbao za kuezekea hivyo unaweza kutoa kutokana na uwezo wako ulionao.

Kwa mawasiliano zaidi na maekekezo tafadhali piga namba hizi hapa.

0774848800 0712550666

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.