Habari za Punde

Kamati ya Baraza la Wawakilishi yafanya ziara kuangalia miradi ya mazingira

Waziri wa Nchi (OMKR) Mhe. Harusi Said Sleiman akimsikiliza mwenyekiti wa kikundi cha Hifadhi ya Mazingira Kikobweni HIMAKI wakati akizungumza kuhusu chanzo cha maji kilichopo Kikobweni mara walipotembelewa na kamati ya Baraza la wawakilishi ya   kusimamia Ofisi za Viongozi wakuu wa Kitaifa kuangalia miradi ya Mazingira . PICHA NA FAUZIA MUSSA-MAELEZO ZANZIBAR 

 

Wajumbe wa Kamati Baraza la wawakilishi ya   kusimamia Ofisi za Viongozi wakuu wa Kitaifa wakiangalia Chanzo cha Maji kilichopo Kikobweni Kinachotunzwa na kuhifadhiwa na kikundi  cha Hifadhi ya Mazingira Kikobweni HIMAKI huko Chaani  Wilaya ya Kaskazini "A"Mkoa WA Kaskazini Unguja . PICHA NA FAUZIA MUSSA-MAELEZO ZANZIBAR 
Mwenyekiti wa kamati ya Baraza la wawakilishi ya   kusimamia Ofisi za Viongozi wakuu wa kitaifa Mhe. Machano Othman Said akizungumza na wanakikundi cha Hifadhi ya  mazingira  Kikobweni HIMAKI wakati wa Ziara ya Kamati hiyo   kutembelea miradi ya mazingira Wilaya ya Kaskazini "A"Mkoa wa  Kaskazini Unguja . PICHA NA FAUZIA MUSSA-MAELEZO ZANZIBAR 

Mkurugenzi Idara ya Mazingira OMKR  Farhat  Ali  Mbarouk akizungumza kuhusiana na miradi ya mazingira wakati wa ziara ya Kamati ya kusimamia Ofisi za Viongozi wakuu wa kitaifa kuangalia miradi hiyo huko Wilaya ya Kaskazini "A" Mkoa wa Kaskazini Unguja.ziara hiyo iliongozwa na Waziri wa Nchi OMKR Mhe. Harusi Said Sleiman. PICHA NA FAUZIA MUSSA-MAELEZO ZANZIBAR 

 

Mdau wa Mazingira na Mbunge wa Jimbo la Chaani Mhe.Juma Usonge Hamad akizungumza wakati wa Ziara ya Kamati ya Baraza la Wawakilishi ya kusimamia Ofisi za viongozi wakuu wa kitaifa kuangalia miradi ya mazingira Wilaya ya Kaskazini "A" Mkoa wa Kaskazini Unguja, kamati hiyo iliambatana na Waziri wa Nchi (OMKR)  Mhe.Harusi Said Sleiman PICHA NA FAUZIA MUSSA-MAELEZO ZANZIBAR

Makamo Mwenyekiti kamti ya kusimamia Ofisi za Viongozi wakuu wa kitaifa    Mhe Mtumwa Pea akipanda mti katika Shamba la kikundi cha Hifadhi ya Mazingira Kikobweni  (HIMAKI) wakati walipofanya Ziara kutembelea miradi ya Mazingira huko Chaani Wilaya ya Kaskazini “A”Mkoa wa Kaskazini Unguja .PICHA NA FAUZIA MUSSA-MAELEZO ZANZIBAR 


Na Rahima Mohamed  Maelezo  09/8/2022

 

Mwenyekiti wa Kamati ya Baraza la Wawakilishi ya kusimamia Ofisi za viongozi wakuu wa kitaifa Mhe Machano Othman Said amewataka watendaji wa mazingira kuhakikisha kuwa sheria za mazingira zinafuatwa katika kuwalinda wanavikundi wanaojihusisha na utunzaji wa mazingira.

 

Akizungumza mara baada ya kutembelea kikundi  kinachojishughulisha na kuhifadhi vyanzo vya maji pamoja na utunzaji wa  mazingirahuko  Chaani   Kikobweni  (HIMAKI ) amesema ,kuwepo kwa sheria hizo kutawasaidia wanavikundi  kufanya kazi zao  za kutunza mazingira kwa ufanisi .

 

Aidha Mwenyekiti huyo ameiomba Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais kushirikiana  na Wizara ya kilimo Umwagiliaji Mali asli na Mifugo kuwaelimisha wakulima kupanda miti inayofaa  katika maeneo yaliyopo karibu na vyanzo vya maji ili kuzuia vyanzo hivyo visiathirike na  kukauka.

 

Mhe. Machano ameisisitiza  Ofisi ya Mkoa  kuhakikisha kwamba eneo hilo linalindwa, kuhifadhiwa na kupandwa miti yenye kuleta tija ili kuepuka uvamizi  na kuongezeka kwa uharibifu katika vyanzo vya maji.

 

Nae Waziri  wa Nchi  Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais Mhe Harusi Said Suleiman amesema Wizara yake imejipanga kupanda miti  katika wilaya zote za Unguja na Pemba, kuviimairisha vitalu vya awali ili kuweza kuhifadhi mazingira na kuepuka athari za na mmong’onyoko wa ardhi nchini.

 

Waziri huyo amekipongeza kikundi hicho kwa juhudi wanazochukua za kulinda mazingira  na kuwataka wasivunjike moyo na baadhi ya watu wasiopenda maendeleo  ili kuleta manufaa  kwa vizazi vijavyo.

 

 

Nae Katibu Tawala wa Mkoa huo Makame Machano Haji amesema atahakikisha wanasimamia vyema  kwa kuwapatia elimu na kuwaunga mkono katika masuala ya utunzaji wa mazingira.

 

Akisoma Risala ya Mjumbe wa  kikundi cha Himaki Mwanaisha Makame Abdalla wamesema kikundi hicho kinakabiliwa na changamoto ya kuvamiwa na watu wanaolima katika maeneo ya hifadhi pamoja na matumizi mabaya katika vyanzo vya maji.

  

Kamati hiyo imetembelea kikundi cha HIMAKI na mradi wa majiko nafuu katika  Wilaya ya Kaskazini “A” Mkoa wa Kaskazini Unguja.

 

 

 

 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.