Habari za Punde

Kikosi cha Zimamoto Zanzibar Wafanikiwa Kuudhibiti na Kuuzima Moto Katika Mtaa wa Kiponda.Katika Ajali Hiyo Mtu Mmoja Amefariki Dunia na Mtoto Kujeruhiwa na Kukimbizwa Hospitali ya Mnazi Mmoja.a oo Moto Matukio ya Picha Ajali ya Moto Mtaa wa Kiponda Unguja leo na Mtu Mmoja Amefariki Dunia na Watoto Wawili Wajeruhiwa Katika Ajali Hiyo

Askari wa Kikosi cha Zimamoto Zanzibar wakiwa takita zoai la kuuzima moto  wakati nyumba moja katika Mji Mkongwe wa  Zanzibar ikiwaka moto.
Kikosi cha Jeshi la Zimamoto wamefanikiwa kuudhiniti moto huo  na kufanikiwa kuuziwa  kunusuru majengo mengi karibu na jengo hilo  na kupata changamoto nyingi kutokana hali ya mazingira ya eneo hilo.
Mwanchi aliyefariki ni mkaazi wa nyumba hiyo Bi. Rehema Chande alijaribu kujiokoa kwa kuruka nje akiwa na mtoto wake na kumkuta mauti na Mtoto wake Nabil Issa amepata majaraha na kukimbizwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja kwa ajili ya kupata huduma ya kwanza, kwa mujibu wa Wananchi walioshuhudia tukio hilo.
Wananchi wakifuatilia zoezi la uzimaji wa moto katika nyumba moja iliyoko katika mtaa wa mji mkongwe Kiponda Wilaya ya Mjini Unguja ikiwaka moto, katika zoezi hilo kikosi cha Zimamoto Zanzibar wamefanikiwa kuuzima moto huo leo 30-8-2022.  

Askari wa Kikosi cha Zimamoto Zanzibar wakiendelea na zoezi la uzimaji wa moto katika nyumba moja iliyopata ajali hiyo katika mtaa wa Kiponda Mji Mkongwe wa Unguja Jijini Zanzibar leo 30-8-2022. 
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe.Idrisa Kitwana Mustafa akipata maelezo kutoka kwa Sheha wa Kiponda alipofika katika eneo la jali hiyo katika mtaa wa kiponda leo kutembelea na kuwafariji Wananchi waliopata maafa hayo ya kuunguliwa na kupata msiba wa ndugu yao Marehemu Rehema Chande, kutokana na ajali hiyo ya moto iliyotokea leo majira ya asubuhi. 
Mstahiki Meya wa Jiji la Zanzibar Mhe. Mahmoud Mussa akiwa  na Mkuu wa Wilaya ya Mjini Unguja Mhe. Rashid Msaraka wakitembelea eneo la ajali ya moto mtaa wa kiponda na kuwafariji wananchi waliopata mafaa hayo leo. 

KAMISHNA wa Kikosi cha Zimamoto na Uokozi Zanzibar Rashid Mzee Abdalla akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali Zanzibar baada ya kukamilika kwa zoezi la uzimaji wa moto katika mtaa wa Kiponda Mji Mkongwe Jijini Zanzibar, Kikosi chake kimefanikiwa kuudhibiti moto huo kutoleta madhara kwa majengo ya jirani na nyumba hiyo iliyopata ajali ya moto.
kulikuwa na changamoto za hapa na pale kutokana na mazingira ya mitaa hiyo ya Mji Mkongwe wa Zanzibar. 


Jengo lililopata ajali ya kuungua kwa moto katika mtaa wa kiponda jirani na skuli ya Hurumzi  kama linavyoonekana baada ya kukamilika kwa zoezi la uzimaji wa moto huo na Kikosi cha Zimamoto Zanzibar leo.
 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.