STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 26 Agost,2022
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema Zanzibar inawahitaji
Wawekezaji kutoka Jamuhuri ya Kiislamu ya Iran, kuja nchini kwa ajili ya kuwekeza katika sekta mbali mbali za Uchumi wa
Buluu.
Dk. Mwinyi amesema hayo Ikulu
Zanzibar, alipokutana na Ujumbe kutoka Serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran,
ulioongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje ya Nchi hiyo Hossein Amir Abdollahian, ambapo pamoja na
mambo mengine mkutano huo ulibainisha maeneo mbali mbali ambapo nchi hiyo
inalenga kuisaidia Zanzibar.
Alisema Zanzibar ina sera nzuri za
Uwekezaji, huku ikiwa na mahitaji makubwa ya kupata wawekezaji katika sekta ya
uchumi wa buluu ili kuimarisha uchumi wake.
Aidha, aliwataka wataalamu wa nchi
hiyo kuja nchini kuangalia namna ya kuimarisha sekta za uvuvi pamoja na
biashara.
DK. Mwinyi alilipongeza Taifa kwa
mashirikiano ya kihitoria kati yake na Zanzibar pamoja na kusaidia juhudi za
Serikali katika kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii, katika nyanja mbali
mbali ikiwemo biashara, vyuo vya amali, kilimo, utibabu na madawa.
Alisema Zanzibar ina mahitaji makubwa
ya nishati hya umeme, ambapo hivi sasa inapata huduma hizo kupitia Waya wa
chini ya Bahari (marine Cable) kutoka Tanzania Bara, hivyo amepongeza azma ya
Iran inayolenga kushirikiana na Zanzibar kupitia sekta hiyo.
Aidha, Dk. Mwinyi alishukuru Iran kwa
kuazimia kushirikiana na Zanzibar katika suala la upatikanaji wa fursa za masomo
nje ya nchi (scholarship), na kusema ni jambo jema litakalowawezesha wanaafunzi
wa Zanzibar kujifunza, hususan katika masomo ya Sayansi.
Rais Dk. Mwinyi aliiomba Iran kuleta
watendaji wake ili kukaa pamoja na wenzao wa Zanzibar ili kuona kwa namna gani
wataweza kusaidia uimarishaji wa sekta
za Viwanda ili kutoa fursa za ajira kwa vijana pamoja na kutaka wataalamu wa
nchi hiyo kuja kuanzisha viwanda hivyo.
Ailipongeza juhudi zilizoanza
kuchukuliwa na Taifa hilo za kusaidia uimarishaji wa sekta ya kilimo kwa kuipatia
Zanzibar zana na vifaa mbali mbali ikiwemo Matrekta pamoja na ‘Power Tiller’ ili kuendeleza kilimo cha
kisasa.
Aidha, alitoa shukrani kwa mualiko
aliopewa kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Ebrahim Raissi wa kulitembelea Taifa hilo
hapo baadae.
Mapema, Waziri wa Mambo ya Nje wa
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Hossein Amir Abdollahian alibainisha maeneo mbali
mbali ambapo Taifa hilo linalenga kushirikiana na Zanzibar, ikiwemo suala la kuendeleza
ushirikiano uliopo kati ya Watu wa Jamii ya Shirazi walioko Iran na wale wa
Zanzibar.
Alieleza kuwa Iran ina azma ya
kuanzisha ushirikiano na Zanzibar katika suala la upatikanaji wa Nishati na
kusema nchi hiyo ina uzoefu mkubwa katika suala la Nishati ya umeme, huku
akatolea mfano wa mradi mkubwa unaoendelea
kutekelezwa na Taifa hilo nchini Iraq unaohusisha umeme wa Megawati 4000.
Hossein alisema eneo jengine ambalo taifa hilo linalenga
kushirikiana an Zanzibar ni la upatikanaji wa fursa za masomo nje ya nchi, ili
kuwawezesha wanafunzi wa Zanzibar kwenda nchini humo kujifunza katika nyanja
mbali mbali za kitaalamu.
Aidha, alieleza eneo jengine ambapo Irani inaweza kushirikiana
na Zanzibar ni juu ya ujenzi wa miundombinu, ukihusisha ujenzi wa barabara, njia
za reli pamoja na viwanja vya ndege.
Kuhusiana na sekta ya Biashara, Waziri
huyo alisema ni eneo ambalo Taifa hilo
liko tayari kushirikiana na Zanzibar, na kusema nchi hiyo inashika nafasi ya
tano Duniani.
Katika hatua nyengine, Waziri Hossein
alitoa mapendekezo kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kuitaka kuandaa
Kamati ya Jumuiya ya Wafanya Biashara kwa lengo la kubainisha maeneo yanayopasa
kushirikiana.
Aliahidi kuendeleza ushirikiano
uliopo kati ya nchi mbili hizo katika sekta za Utalii, uchumi wa Buluu, Afya,
pamoja na kuandaa majukwaa
yatakayofanikisha kufanyika uchambuzi ili kubaini fursa za ushirkiano.
Aidha, alitoa pendekezo linalotoa
nafasi ya kuwajengea uwezo wataalamu wa Zanzibar pamoja na kutoa fursa ya
kuwakutanisha na wenzao wa Iran kwa lengo la kupata uzoefu katika nyanja
za elimu ya juu pamoja na Sayansi.
Alisema Taifa hilo lina azma ya
kuanzisha Chuo kikuu hapa nchini ili kutoa fursa kwa wanafunzi wazalendo
kujifunza nyanja mbali mbali ambazo Serikali ina mahitaji makubwa, kama vile
sekta ya mafuta na gesi asilia.
“Pendekezo jengine ni la kubadilisha uzoefu katika
shughuli za Mabunge hususan katika Dilomasia ya Uchumi”, alisema.
Imetayarishwa na Idaya ya Mawasiliano
Ikulu Zanzibar.
No comments:
Post a Comment