Dodoma Tarehe: 9 Agosti 2022
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Ndugu Wanahabari, awali ya yote nianze kwa kumshukuru Mwenyezi
Mungu ambaye ametuwezesha kukutana nanyi siku hii ya leo tukiwa na afya njema.
Ndugu zangu Waandishi wa Habari tumewaita hapa leo kwa ajili ya kueleza
utekelezaji wa shughuli za Shirika la Nyumba la Taifa na Mwelekeo wa
utekelezaji kwa mwaka wa fedha 2022/2023.
Shirika la Nyumba la Taifa lilianzishwa mwaka 1962 kwa sheria Na.45 likiwa na jukumu la kuwezesha ujenzi wa nyumba na majengo mengine kwa matumizi mbalimbali hususan makazi, Ofisi na biashara. Mwaka 1990 Shirika hili liliunganishwa na iliyokuwa Msajili wa Majumba(Rob) iliyoanzishwa mwaka 1971 kwa sheria Na. 13 ili kusimamia majumba yaliyotwaliwa na serikali. Ili kulifanya Shirika hili kujiendesha kibiashara mapitio ya sheria ya NHC ya mwaka 1990 na sheria ya ardhi Na.4 ya mwaka 1999 yalifanyika mwaka 2005 kupitia sheria Na. 2.
Majukumu ya Shirika yanatekelezwa
kwa kuzingatia Mpango Mkakati wa Shirika
wa Miaka 10 (2015/16 – 2024/25) ambao unalenga kusukuma mbele ujenzi wa
nyumba zipatazo 10,000 na kuwezesha ukuaji wa sekta ya nyumba kupitia
ushirikishwaji wa sekta binafsi.
Shirika la Nyumba lina mtaji(capital base) wa Shilingi trilioni 5.04 hivi sasa unaotokana na rasilimali ya majengo yake 2,650 yenye nyumba(Units) zipatazo 18,654 zilizopo katika mikoa mbalimbali nchini.
MIRADI ILIYOTEKELEZWA KATIKA MWAKA WA FEDHA
2021/22 NI KAMA IFUATAVYO:-
(a)Ujenzi wa Nyumba
1.
Katika mwaka 2021/22, Shirika lilipanga kukamilisha Mradi wa Morocco Square Jijini Dar es Salaam. Napenda kuwataarifu kuwa hadi
tarehe 30 Juni, 2022, utekelezaji wa Mradi huo umefikia asilimia 94.
- Ili
kukamilisha mradi huu uliosimama tangu 2018 kwa kukosa fedha, Serikali imeruhusu
Shirika kukopa fedha za kukamilisha mradi huu na miradi mingine ikiwemo Kawe
711. Mpaka sasa Shirika limekopa shilingi bilioni 44.7 kwa ajili hiyo. Mradi
wa Morocco Square utakamilika Desemba
2022.
2. Mradi wa ukandarasi wa Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa Mwalimu Nyerere (Mara) Awamu ya IV umekamilika kwa asilimia 99 na Mradi wa ujenzi wa Soko la Kimataifa la Mifugo la Buzirayombo (Geita) umekamilika kwa asilimia 100 na tumeukabidhi.
(b) Uandaaji wa
Mipango Kabambe
Mwaka 2021/22, Shirika lilitekeleza Mpango wa uandaaji wa Mipango Kabambe ya Uendelezaji wa
maeneo ya Kwala (Pwani) na Mji wa
Tanzanite wa Mirerani (Manyara). Aidha, uandaaji wa Mpangokina kwa ajili ya
uendelezaji wa maeneo ya Chuo Kikuu cha Dodoma ulifanyika na unaendelea.
(c) Ujenzi wa Viwanda
vya Vifaa vya Ujenzi
Ili kutimiza azma ya kujenga nyumba za gharama nafuu nchini hususan kwa
ajili ya wananchi wa kipato cha chini, hadi tarehe 30 Juni, 2022, Shirika limenunua maeneo kwa ajili ya uchimbaji mchanga na uzalishaji wa kokoto. Mpango wa Shirika ni kuhakikisha viwanda vya
uzalishaji wa vifaa vya ujenzi kutosheleza miradi yake na baadae watanzania
wengine unaanza kutekelezwa kwa siku zijazo.
(d) Ukarabati wa
Nyumba
Ndugu Wanahabari, sambamba na ukusanyaji
wa kodi ya nyumba, Shirika limeendelea kufanya ukarabati wa nyumba zake kupitia Mpango Maalum wa
Ukarabati. Katika mwaka 2021/22, Shirika llilitumia shilingi bilioni 3 kukarabati nyumba 180 katika mikoa ya Kilimanjaro, Dar es
Salaam na Katavi.
- Ndugu Wanahabari, katika siku 100 za Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Bw. Nehemiah Kyando Mchechu
tangu alipoteuliwa mambo kadhaa yamefanyika ikiwemo kufanya mikutano ya
mashauriano(engagements) na wadau
muhimu wa sekta ya nyumba ili kupata
uelewa wa pamoja wa sekta na uungwaji mkono. Kazi hiyo imeshakamilika kwa
mafanikio makubwa.
Katika mwaka 2022/23, Shirika litatumia
shilingi bilioni 413.7 kutekeleza vipaumbele
vifuatavyo:-
i)
Kutekeleza
Mpango wa ujenzi wa nyumba 5000 za gharama ya kati chini ujulikanao Samia Housing Scheme (SHS). Mradi huu
wa nyumba za kuuza na kupangisha unakusudia kuenzi kazi nzuri anazofanya
Mheshimiwa Rais na tunatamani watanzania waje wamkumbuke kwa miaka mingi ijayo.
Asilimia 50 ya nyumba hizi zitajengwa Dar esSalaam, Dodoma asilimia 20 na mikoa
mingine asilimia 30. Nyumba hizi zitaanza kujengwa mwezi Septemba eneo la Kawe Dar
es Salaam (nyumba 500) na Medeli Jijini
Dodoma (nyumba100). Mradi huu
utakaotekelezwa kwa awamu utagharimu takriban Shilingi bilioni 466 sawa na dola za
Kimarekani milioni 200.
ii)
Kukamilisha
ujenzi wa Mradi wa Morocco square
ambao ujenzi upo kwenye hatua ya uboreshaji wa mandhari
(landscaping na ufungaji wa lifti na
viyoyozi kazi ambazo kufikia mwezi Desemba 2022 zitakamilika. Aidha, sambamba
na ujenzi huo, Shirika litaendelea na kukamilisha miradi ya Kawe 711 na Golden Premier Residence
(GPR) iliyopo Kawe.
iii)
Kuanza utekelezaji wa Sera ya Ubia itakayoruhusu Sekta Binafsi kushiriki katika
uendelezaji wa maeneo ya Shirika. Sera hii ina lengo
la kuharakisha uendelezaji wa maeneo yaliyo wazi katikati ya miji yetu kwa
kujenga nyumba za vitega uchumi na hivyo kuliongezea Shirika na nchi mapato
makubwa. Mpango huu unaounga mkono sera
ya Mheshimiwa Rais ya kuvutia uwekezaji nchini, utazinduliwa Septemba 2022 na
mtaarifiwa.
v)
Kuendelea na utekelezaji wa miradi ya
ukandarasi ikiwemo ujenzi wa Majengo ya
Ofisi za Wizara nane (8) Jijini
Dodoma, ujenzi wa Jengo la Shule ya
Uchumi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Ujenzi
wa majengo matano (5) ya Wakala wa Ununuzi wa Serikali (GPSA), ujenzi wa jengo la
TANZANITE Mirerani, ujenzi wa Jengo la
Kitengo cha Moyo cha Jakaya Kikwete (JKCI) na miradi mingine itakayojitokeza;
vi)
Kuendelea kukusanya
mapato na kodi ya pango ya nyumba
za Shirika. Tunatoa
wito kwa wapangaji na wadaiwa sugu wa kodi ya pango kuhakikisha wanalipa kodi
na malimbikizo wanayodaiwa kwa kuwa Shirika kuanzia sasa linajiandaa kukusanya
kodi hii kwa asilimia 100.
vii)
Kuendelea kutekeleza Mpango Maalum wa miaka mitano wa ukarabati
wa nyumba za Shirika unaoishia
mwaka 2027, kukarabati nyumba katika
mikoa ya Dar es Salaam, Iringa, Tabora,
Arusha, Kigoma, Morogoro, Lindi, Tanga, Mbeya, Mwanza, Singida na Kagera
kwa gharama ya shilingi bilioni nane (8).
viii)
Kusaidiana na Wizara na wadau wa sekta ya
Miliki nchini kubuni sera na sheria zitakazoifanya sekta ya miliki na nyumba
kuchangia uchumi wa nchi yetu. Kazi hii
tumeshaianza.
ix)
Kuendelea
na ujenzi wa viwanda vya kuzalisha vifaa vya ujenzi wa nyumba za NHC hususan
kokoto na matofali;
x)
Kununua ardhi ekari
400 katika maeneo mbalimbali ya kimkakati kwa ajili ya
ujenzi wa nyumba na akiba ya ardhi;
xi)
Tunaendelea
kuhamasisha wananchi na wapangaji wetu kujitokeza Agosti 23, 2022 kuhesabiwa.
Sensa ya watu na makazi ni kwa ajili ya kuleta maendeleo.
xii)
Kuendelea kushirikiana na vyombo
vya habari kutoa elimu kwa umma kuhusu masuala ya nyumba na Sekta
ya Milki nchini. kupitia vyombo vya habari; vyombo vya habari ni
mhimili muhimu wa upashanaji habari kwa Wananchi, uelimishaji na kujenga
taswira ya Shirika.
1.
Kutoa ajira kwa watanzania- mradi wa SHS
wa nyumba 5000 pekee unatarajiwa kutoa ajira zipatazo 26,400(direct 17,600 na indirect 8,800)
2.
Kukuza mapato ya serikali mfano mradi
wa SHS 5000 unatarajiwa kutengeneza mapato ya kodi mbalimbali za serikali TZS bilioni 50 (mauzo ya nyumba) bilioni 10( ununuzi vifaa vya ujenzi), PAYE TZS 17.8 bilion, Kodi ya majengo TZS milioni 55, corporate Tax kutoka
NHC na wajenzi wengine bilioni 77,
VAT 60bilioni
3.
Kukuza sekta ya fedha kupitia mikopo
ya nyumba watengenezaji, wauzaji na wakondarasi watakopa asilimia hadi 60
ambayo ni sawa na TZS 194.8 bilioni(SHS)
4.
Kukuza soko la sekta za huduma kama
umeme, maji, gesi, simu, media (matangazo), ulinzi nk
5.
Kuongeza maisha bora kwa wananchi.
Taarifa ya UN Habitat ya hali ya Idadi ya watu, inasema kuwa asilimia 50 ya
watu waliishi mijini mwaka 2020 na ifikapo 2050 idadi ya watakaokuwa wakiishi
mijini itafikia 70%. Tanzania itakuwa na watu135m na mwaka 2100 itakuwa na watu
286m na kuwa nchi ya 9 duniani. Hii inahitaji mipango madhubuti ya kupanga miji
na upatikanaji wa nyumba.
6.
Tunatekeleza Ilani ya Uchaguzi Ibara
ya 75
7.
Kukuza ukuaji wa Viwanda - sementi, mbao, kokoto nondo marumaru
mitambo(concrete mixers) vioo, samani, mabati, bomba na umeme
8.
Kuwa na mandhari nzuri na miji
iliyopangwa- 70% ya miji yetu haijapangwa
9.
Kudumisha amani na
utangamano-kupunguza uhalifu mijini, rejea Kibera, Nairobi 2012
Muungano
Kasibi Saguya
SHIRIKA
LA NYUMBA LA TAIFA
No comments:
Post a Comment