Habari za Punde

Waandishi wa Habari Wapatiwa Elimu ya Kinga ya Saratani ya Shingo ya Kizazi.

Baadhi ya Waandishi wa Habari wakimsikiliza Mkufunzi kutoka  Kitengo cha Maradhi Yasioambukiza, Hospitali ya Rufaa Mnazi mmoja Omar Abdalla Ali (hayupo pichani) juu ya ongezeko la saratani ya chingo ya kizazi hapa nchin, katika Ofisi za Muungano wa  Watu wanaoishi na Maradhi yasioambukiza, Mpendae.
Mratibu wa Kitengo cha Maradhi Yasioambukiza kutoka Hospitali ya Rufaa Mnazi mmoja Omar Abdalla Ali  akielezea ongezeko la Saratani ya Shingo ya Kizazi kwa Akinamama na vichocheo vyake kwa waandishi wa habari katika Jumuiya ya Watu Wanaoishi na  Maradhi Yasioambukiza, Mpendae .

Na Khadija Khamis – Maelezo.

Ugonjwa wa Saratani  ya Shingo  ya Kizazi umekua ukiongezeka kwa kasi siku hadi siku na kupelekea kuwaathiri wanawake wengi hapa nchini.

 

Akizungumza katika Mkutano na Waandishi wa Habari juu ya elimu ya kinga ya Saratani ya Shingo ya kizazi kwa wanawake,  Mratibu wa Kitengo cha Maradhi Yasioambukiza kutoka Hospitali ya Rufaa Mnazi mmoja Omar Abdalla Ali amesema maradhi haya yamekuwa yakiongezeka kwa kasi kubwa hapa nchini.

 

Amesema shingo ya kizazi inazuilika au kutibika endapo itagundulikana  mapema ikiwa kwenye hatua za awali hivyo ni muhimu kufanya uchunguzi wa afya mara kwa mara pamoja na kufuata ushauri wa wataalamu wa afya 

 

wanawake wote walio na umri wa miaka 30 na kuendelea wanatakiwa  kufanya uchunguzi wa saratani ya shingo ya kizazi japo kwa mwaka mara moja

 

Mratibu huyo amewataka wanawake  kuacha kutumia kemikali  za aina yoyote  kuweka katika sehemu ya uke jambo ambalo  huathiri  njia  ya kizazi na kupeleka kupata saratani ya shingo ya kizazi.

 

Nae Meneja wa Muungano wa Watu  Wanaoishi na Maradhi Yasioambukiza  Zanzibar  (NCDs) Haji Khamis Fundi ameitaka jamii hasa wanawake kufanya uchunguzi  na kuachana na vichecheo vinavyosababisha maradhi hayo.

c

Aidha alisema kukosa elimu ya kujiepusha na Saratani kwa jamii kunachangia kuwepo na kesi nyingi za ugonjwa huwo hivyo aliishauri jamii kujiepusha na vichocheo vya maradhi hayo

 

Hata  hivyo aliitaka  jamii  kuacha  matumizi ya vyakula  vyenye  kemikali   nyingi na vile vya makopo vilivyopita  muda wake, matumizi ya tumbaku,   sigara,  pombe na utiaji wa vitu visivyofaa sehemu za siri  pamoja na matumizi ya mionzi ya mara kwa mara.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.